Home BUSINESS WAZIRI MKUU AFUNGUA SEMINA MAALUM KATIKA SEKTA YA KILIMO

WAZIRI MKUU AFUNGUA SEMINA MAALUM KATIKA SEKTA YA KILIMO

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akifuatilia mada   kabla ya kufungua Semina Maalum ya Uwekezaji katika Sekta ya Kilimo iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwenye ukumbi wa  The Super Dome , Oysterbay jijini Dar es salaam, Aprili 28, 2024. Kulia kwake ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega na kushoto kwake ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid Nsekela.  (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza na Wakurugenzi wa Kampuni ya utengenezaji  bidhaa za ngozi iitwayo  Fay Fashion , Bw. Geofrey Mlay (kushoto) na mkewe Faith Mlay alipotembelea banda lao la maonesho kabla ya kufungua  Semina Maalum ya Uwekezaji katika Sekta ya Kilimo iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwenye ukumbi wa  The Super Dome , Masaki jijini Dar es salaam, Aprili 28, 2024. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akisalimiana na viongozi  mbalimbalia liopwasili kwenye ukumbi wa The Super Dome, Masaki jijini Dar es salaam kufungua Semina Maalum ya Uwekezaji katika Sekta ya Kilimo iliyoandaliwa na Benki ya CRDB, Aprili 28, 2024. (Picha naOfisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu ng’ombe kutoka kwa Collins Seronga alipotembelea banda la Chama cha Wafugaji Tanzania kabla ya kufungua Semina Maalum ya Uwekezaji katika Sekta ya Kilimo iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwenye ukumbi wa  The Super Dome , Oysterbay jijini Dar es salaam, Aprili 28, 2024. Kulia kwake ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akitazama uyoga alipotembelea banda la Kampuni ya Dorkin Organic Farming kabla ya kufungua Semina Maalum ya Uwekezaji katika Sekta ya Kilimo iliyoandaliwa na Benki ya CRDB kwenye ukumbi wa  The Super Dome , Oysterbay jijini Dar es salaam, Aprili 28, 2024. Kushoto ni Waziri wa Mifugo na Uvuvi, Abdallah Ulega na kulia ni Mkurugenzi Mtendaji wa Benki ya CRDB, Abdulmajid  Nsekela. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Aprili 28, 2024 amekuwa mgeni rasmi katika Semina Maalum ya uwekezaji katika kilimo iliyoandaliwa na benki ya CRDB katika Ukumbi wa The Super Dome Masaki.

Semina hiyo imewakutanisha wadau wa sekta ya kilimo, mifugo, uvuvi pamoja nawazalishaji wa zana za kilimo na mifugo.

Mheshimiwa Majaliwa pia ametembelea mabanda mbalimbali ya maonesho yaliyoko katika viwanja vya ukumbi huo.

Previous articleTUSIWATENGE WALA KUWANYANYAPAA WATOTO WENYE USONJI – MAJALIWA
Next articleWAZIRI MKUU KUSHUHUDIA UTIAJI SAINI MIKATABA 20 YA MIRADI YA UMWAGILIAJI
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here