Home BUSINESS RC MTAKA ATEMBELEA BANDA LA BRELA

RC MTAKA ATEMBELEA BANDA LA BRELA

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka, (wa pili kushoto), akitia saini katika kitabu cha wageni alipotembelea  Banda la Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) wakati wa ziara yake ya kutembelea Mabanda ya washiriki, katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Nanenane yanayofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale  Jijini Mbeya, leo Agosti 4,2023.

Kiongozi huyo, ametembelea Banda la BRELA kujionea shughuli wanazofanya na kuitaka BRELA kuongeza jitihada katika kuhamasisha wadau kurasimisha Biashara zao ili kukuza uchumi wa nchi.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka (kushoto),  akipata maelezo kuhusu wageni wanaotembelea Banda la BRELA kutoka kwa Mkuu wa Kitengo cha Habari na Mawasiliano BRELA, Bi. Rhoida Andusamile (wa pili kushoto) alipofanya ziara katika Banda la Wakala huyo, kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Nanenane, Agosti 4, 2023 Jijini Mbeya.

Mkuu wa Mkoa wa Njombe Mhe. Anthony Mtaka, akiwa katika picha ya pamoja na baadhi ya watumishi wa BRELA katika Maonesho ya Nanenane Jijini Mbeya.

Previous articleRC MTAKA ATEMBELEA BANDA LA MKEMIA MKUU WA SERIKALI MAONESHO YA NANENANE JIJINI MBEYA
Next articleVETA KUPANUA MAFUNZO YA UFUNDI SIMU NCHINI
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here