Home LOCAL TET YAWASILISHA MADA YA UBORESHAJI WA MITAALA YA ELIMU KWA UMOJA WA...

TET YAWASILISHA MADA YA UBORESHAJI WA MITAALA YA ELIMU KWA UMOJA WA WAKUU WA SHULE ZA KIKRISTO ‘CSSC’


Na: Mwandishi Wetu, Dodoma.

TAASISI ya Elimu Tanzania (TET), mapema leo Januari 25,2022 imewasilisha mada juu ya uboreshaji wa Mitaala ya Elimu ya Awali, Msingi, Sekondari na Elimu ya Ualimu katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Wakuu wa Shule za Kikristo Tanzania (CSSC).

Wasilisho hilo limetolewa na Mkurugenzi Mkuu wa TET, Dkt. Aneth Komba  katika Mkutano huo unafanyika  katika ukumbi wa St Gasper Jijini Dodoma  ulioanza kuanzia tarehe 24 ambapo utafikia tamati Januari 28 mwaka huu.

Baada ya wasilisho hilo kutoka kwa Dkt. Komba walimu hao walipata nafasi ya kutoa maoni yao juu ya uboreshwaji wa Mitaala hiyo.

Zoezi hilo la ukusanyaji wa maoni linatarajiwa kukamilika Januari 31 mwaka huu ambapo mchakato wa kuboresha Mitaala itachukua muda wa miaka 3 na Mitaala mipya inatarajiwa kuwa darasani mwaka 2025.

Mwisho.

Previous articleZANZIBAR WATUMIA TEKNOLOJIA YA HARAKA ‘AKILI BANDIA’ KUPIMA UVIKO 19, MAJIBU NDANI YA SEKUNDE MOJA
Next articleFEDHA ZA REGROW KUBORESHA HIFADHI YA TAIFA MIKUMI
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here