Home LOCAL TMD YAWATAKA WAKAGUZI VIWANDA VYA DAWA KUFUATA MAADILI

TMD YAWATAKA WAKAGUZI VIWANDA VYA DAWA KUFUATA MAADILI

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba  TMDA Adam Fimbo akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Kando ya Mafunzo ya ukaguzi kwa wafanyakazi wa Mamlaka hiyo yanayofanyika kwenye ofisi za taasisi hiyo Mabibo jijini Dar es Salaam.

Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba  TMDA Adam Fimbo akifafanua jambo wakati  akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Kando ya Mafunzo ya ukaguzi kwa wafanyakazi wa Mamlaka hiyo yanayofanyika kwenye ofisi za taasisi hiyo Mabibo jijini Dar es Salaam.

Mkaguzi na Mchambuzi wa Maabara kutoka Kanda ya Ziwa Bw. Bugusu Mweru ambaye ni mshiriki wa mafunzo hayo akieleza kwa waandishi wa habari umuhimu wa mafunzo hayo kwa wakaguzi wa TMDA.

DAR ES SALAAM 

Mamlaka ya Dawa  na vifaa tiba TMDA imewataka wakaguzi wa viwanda vya kutengeneza dawa  kufuata maadili kwani wao ndio nguzo kubwa katika kuhakikisha dawa zinazozalishwa zinakidhi vigezo vya kitiba na kiuchunguzi.

Wito huo umetolewa leo Desemba 15,2023 jijini Dar es salaam na Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba  TMDA  Bw. Adam Fimbo wakati akizngumza na waandishi wa habari kuhusu  mafunzo ya siku tano kwa wakaguzi wa viwanda wa taasisi hiyo.

Amesema kwa kutambua umuhimu wa wakaguzi hao katika kuhakikisha wanasimamia ubora wa dawa wameamua kuwapa elimu hiyo ili kuhakikisha viwanda vinatengeneza bidhaa zenye viwango ili kuepusha kuingiza bidhaa duni sokoni ambazo zitaleta athari kwa jamii.

“Sisi kama TMDA kazi ya ukaguzi ni kazi yetu ya msingi hivyo tunafanya ukaguzi kwenye viwanda vinavyotengeneza dawa ili kuhakikisha jamii haipati madhara yanayotokana na  dawa zisiszokidhi viwango kwa matumizi ya binadamu.”Amesema Fimbo.

Amesema TMDA ina jumla ya wakaguzi 45 hivyo wanahitaji wakaguzi zaidi ili kuendelea kufanya kazi hiyo kwa ufanisi ingawa wakaguzi waliopo wanaweza kufikia sehemu zote.

“TMDA tunakagua viwanda,maduka ya jumla na rejereja na maghala hivyo ni lazima tuwe na wakaguzi wa kutosha kwani mpaka sasa wapo 45 kwa asili ya kazi yetu haina shida sana lakini tunahitaji tuwapate wa kutosha zaidi ili watusaidie kufanya ukaguzi”amesema.

Ameongeza kuwa uwepo wa kaguzi hizo umesaidia viwanda hasa vya ndani kuweza kuzalisha bidhaa zenye ubora na viwango vinavyohitajika nchini.

Kwa upande wake mmoja wa wakaguzi ambao wapo kupata mafunzo hayo Bugusu Mweru ambaye ni Mkaguzi na Mchambuzi wa Maabara kutoka Kanda ya Ziwa amesema mafunzo hayo yatawasaidia kwenye kaguzi zao ili kuhakikisha jamii inapata dawa zenye ubora na zilizokidhi vigezo vya kitiba.

Mafunzo hayo ya siku tano yaliyowakutanisha wakaguzi 34 yanalengo la kuwasaidia wakaguzi  kufanya kazi zao kwa weledi na maadili na kukwepa vitendo vya rushwa kwa maslahi mapana ya jamii na Taifa kwa ujumla.

Picha mbalimbali zikionesha washiriki  wakiendelea na mafunzo hayo yanayofanyika kwenye ofisi za TMDA Mabibo jijini Dar es Salaam.

Previous articleSERIKALI IMEJIPANGA KUONGEZA VIRUTUBISHO NA MADINI KWENYE VYAKULA
Next articleMIUJIZA YA NABII JACKSON YAIBUA MAZITO
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here