Home LOCAL TANZANIA KUFUNGUA RASMI OFISI ZA UBALOZI INDONESIA

TANZANIA KUFUNGUA RASMI OFISI ZA UBALOZI INDONESIA

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mhe. Dkt. Stergomena Tax (Mb.) amewasili Jakarta nchini Indonesia kwa ajili ya ziara ya kikazi, ikiwa ni pamoja na kufungua rasmi Ofisi za Ubalozi wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania nchini humo hapo Tarehe 22 Juni, 2023.

Mhe. Dkt. Tax baada ya kuwasili Jakarta amepokelewa na Balozi wa Tanzania nchini Indonesia, Mhe. Macocha Tembele katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Soekarno-Hatta (CGK).

Akiwa nchini Indonesia Mhe. Dkt. Tax anatarajia pia kukutana na kufanya mazungumzo na Waziri wa Mambo ya Nje wa Indonesia, Mhe. Retno Marsudi, na kutembelea Chuo cha Diplomasia cha Indonesia.

Previous articleSUA KUSHIRIKIANA NA SERIKALI YA INDIA 
Next articleKINANA AKUTANA NA BALOZI WA BRAZIL NCHINI TANZANIA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here