Home LOCAL SHAKA ATAKA WANANCHI WAPEWE NAFASI KUSHUHUDIA UTEKELEZAJI WA MIRADI.

SHAKA ATAKA WANANCHI WAPEWE NAFASI KUSHUHUDIA UTEKELEZAJI WA MIRADI.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) ya CCM, Itikadi na Uenezi, Shaka Hamdu Shaka, amewataka viongozi mbalimbali wanaofanya ziara hususan katika miradibya maendeleo kuwapa fursa wananchi kuona kinachofanywa na serikali.

Shaka ameyasema hayo leo jijini Dar es Salaam, alipotembea soko Kuu la Kariakoo akiwa katika ziara ya kikazi kukagua utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM, likiwemo Soko la Kariakoo alikoshuhudia hatua nzuri za ukarabatibwake.

“Ndugu zangu viongozi nadhani sasa ni muda mwafaka kubadilika katika hizi ziara, badala ya kukaa na kujifungia na kuzungumza sisi wenyewe, ni vyema tukawapa nafasi wananchi kuona Yale yanayofanywa na serikali yao chini ya Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema.

Shaka ameipongeza serikali kwa kazi nzuri inayofanya katika ujenzi nabukarabati wa soko hilo ambapo amesema litakapokamilika manufaa yake hayatakuwa kwa Kariakoo pekee bali ni kwa Dar es Salaam na Afrika Mashariki yote.

Awali akimkaribisha Shaka, Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Ludigija Ng’wilabuzu, aliwapongeza wakandarasi wa mradi huo kwa kuutekeleza kwa kasi.

Amesema mradi huo upo chini ya Shirika la Nyumba la Taifa (NHC) ambapo amesema kazi inaendelea vizuri na anaamini itakamilishwa katika muda muda wa makubaliano.

Previous articleJIJI LA DAR ES SALAAM LAJIPANGA KUWA KINARA KWENYE ZOEZI LA SENSA YA WATU NA MAKAZI 2022
Next articleMBUNGE BONAH AFANYA ZIARA KWENYE BARABARA YA CHANG’OMBE-MACHIMBO
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here