Home KIDSNEWS WATOTO 119 WENYE TB WAOKOLEWA

WATOTO 119 WENYE TB WAOKOLEWA

Na: Lucas Raphael,Tabora

 

Serikali imewataka wadau wa Afya nchini kuangalia uwezekano na utaratibu wa Ufuatiliaji wa familia zenye wagonjwa wa kifua kikuu ili  uweza kuleta mafanikio makubwa  na kufanikiwa kuokoa Maisha ya Watoto zaidi ya 119 chini ya miaka mitano waliobainika kuwa na ugonjwa huo baada ya kufanyiwa uchunguzi katika mikoa ya Singida na Tabora.

 

Kauli hiyo ilitoklewa na mkurungezi wa  wa kinga kutoka  wizara ya Afya Dkt.Riziki Kisonga wakati wa kufunga shughuli za mradi wa CAP TB uliokuwa ukitekelezwa katika mikoa ya Tabora na Singida tangu mwaka 2017.

 

Alisema kwamba mradi huo umeweza kufanikisha kuibua wagonjwa wengi wa kifua kikuu chini ya miaka 5 jambo ambalo hapo awali lilikuwa linaondoa uhai wa watoto wengi bila kujulikana .

 

Dkt Kisonga alisema kwamba jitihada zinaendelea kufanywa na serikali katika kukabiliana na ugonjwa wa kifua kikuu uliokuwa chini ya mradi wa CAP TB unaoratibiwa na shirika lisilo la kiserikali la EGPAF.

 

Alisema kwamba mradi huo ulifanikiwa kuwafikia watoto 827,129 kwa uchunguzi  wa kifua kikuu kutoka 335 mwaka 2017 hadi 1852 mwaka huu .

 

Alisema kwamba kuongeza idadi ya watoto walioanzishiwa matibabu ya kifua kikuu kutoka 303 hadi 1851 kwa kipindi hicho kwa vituo vilivyofikiwa .

 

Awali  Mkurugenzi wa Ufundi Shirika la EGPAF Tanzania ,Dkt,Chirspin Kimario alimweleza mkurungezi wa kinga nchini kwamba  wanaishuru serikali ya awamu ya sita kwa jitiada nyingi walizoweka katika kufanikisha huduma za afya ikiwemo ujenzi wa vituo vya afya ,kuweka mazingira wezeshi kwa wagonjwa wa kifua kikuu ili waweze kupata huduma bora za afya stahiki.

 

Hata hivyo walipongeza mpango wa taifa wa kifua kikuu na ukoma kwa kuwapa kipaumbele watoto katika mpango mkakati juu ya kifua kikuu

 

Alisema mradi huo ambao umetekelezwa katika halmashauri 12  za mikoa ya Tabora na Singida na kufikia vituo vya kutolea huduma za afya vipatavyo 45 ikiwemo 17 katika mkoa wa Tabora na 28 mkoani Singida  . 

Previous articleRC KILIMANJARO APOKEA MADARASA 56 YA COVID-19 KATIKA SHULE 36 ZA SEKONDARI WILAYANI SAME
Next articleDC WA ZAMANI TABORA KITWALA KOMANYA AGOMA KUONDOKA MAHAKAMANI KUHOFIA WAANDISHI WA HABARI
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here