Home LOCAL RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AONDOKA NCHINI KUELEKEA MALAWI

RAIS SAMIA SULUHU HASSAN AONDOKA NCHINI KUELEKEA MALAWI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan hii leo Agosti 16, 2021 ameondoka Nchini kuelekea Nchini Malawi kwaajili ya kushiriki Mkutano wa 41 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) utakaofanyika kuanzia tarehe 17-18 Agosti, 2021.

Katika uwanja wa ndege wa Jijini Dodoma , Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan amesindikizwa na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango, Wakuu wa Vyombo vya Ulinzi na Usalama pamoja na viongozi mbalimbali wa Mkoa wa Dodoma wakiongozwa na Mkuu wa Mkoa huo Anthony Mtaka.

 

Previous articleWAZIRI WA TAMISEMI AKAGUA BARABARA NJENGERENDETI HADI UTALINGOLO NJOMBE MJINI.
Next articleRAIS DKT.MWINYI AKUTANA NA BALOZI WA OMAN NCHINI TANZANIA.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here