Home LOCAL DC ILALA AZITAKA BODI ZA SHULE ISIWE UWANJA WA SIASA

DC ILALA AZITAKA BODI ZA SHULE ISIWE UWANJA WA SIASA


NA: HERI SHAABAN

MKUU wa Wilaya ya Ilala Arch ,Ng’wilabuzu Ludigija  amezitaka Bodi za Shule  wasitumie uwanja wa siasa katika kuchaguana kusimamia bodi za shule zilizopo Wilaya ya Ilala .

Mkuu wa Wilaya Ludigija aliyasema hayo Dar es Salaam leo katika semina ya kazi ya Walimu Wakuu wa  shule za sekondari za serikali na binafsi pamoja na Maafisa Elimu Kata kikao kilichoandaliwa na Ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya jiji la Dar es Salam na Idara ya Elimu Sekondari.

“Ninaagiza katika Wilaya yangu  zikaguliwe Bodi za shule kila wakati ziwe hai  pia wasichague wasimamizi wa bodi hizo wanasiasa katika sekta ya elimu “ alisema Ludigija

Ludigija aliwataka Walimu Wakuu na Waratibu Elimu Kata kushirikiana na bodi za shule zao katika kukuza sekta ya elimu ndani ya Wilaya hiyo.

Aliwataka Wakuu wajue majukumu yao na masuala ya uwendeshaji kila Mkuu wa shule anasimamia ipasavyo  ikiwa pamoja na ufundishaji,ujifunzaji kuakikisha mambo yanayowahusu walimu na Watumishi wasio Walimu na haki zao zinasimamiwa na kutekelezwa .

Aliwataka Walimu Wakuu wakae na kufanya tathimini kitaaluma katika mitihani ya ndani na mitihani ya Taifa katika kuweka mikakati yao sekta ya elimu kukuza taaluma Wilaya ya Ilala na kuongeza ufaulu.

Kwa upande wake Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto amewataka Walimu Wakuu wa sekondari na Waratibu Elimu kusimamia fedha za shule na miradi ya shule ya Wilaya ya Ilala

Afisa Elimu Mkoa Dar es Salaam Alhaj Abdul Maulidi aliwataka Walimu wawe na nidhamu sambamba na usimamizi mzuri kwa watoto shuleni .

Alhaj Maulid alisema kazi yao ni wito hivyo wafanye kwa weledi na kudumisha nidham kazini ikiwemo kuboresha mazingira ya shule zao vizuri na kukuza taaluma na kuongeza ufaulu.

Afisa Elimu Sekondari Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Mussa Ally alisema dhumuni la kikao kazi hicho ni maandalizi ya kupokea wanafunzi wa kidato cha kwanza 2022 Walimu Wakuu wa shule za Serikali pamoja na binafsi zilizopo Wilaya ya Ilala .
Mwisho.

 

Previous articleMSHINDI MISS EAST AFRICA 2021 KUONDOKA NA NISSAN X TRAIL YENYE THAMANI YA SH.110,000,000.
Next articleWAKULIMA WA MBAAZI WAENDELEA KUVUNA FEDHA,WANUNUZI PIGANA VIKUMBO NA KUPANDISHA BEI
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here