Home LOCAL SHANTA GOLD YAPONGEZWA KUSIMAMIA LOCAL CONTENT

SHANTA GOLD YAPONGEZWA KUSIMAMIA LOCAL CONTENT


Na. Steven Nyamiti – Singida

Waziri wa Madini Doto Biteko ameeleza kuwa, Mgodi mpya wa Kati wa Dhahabu wa Shanta ndio mgodi pekee Tanzania unaotekeleza ipasavyo Matakwa ya Sheria ya matumizi kwa Jamii husika (Local Content).

Amesema hayo tarehe 30 Julai, 2021 alipotembelea na kukagua Maendeleo ya ujenzi wa Mgodi wa Kati wa Dhahabu wa Singida (SINGIDA GOLD MINE) Shanta uliyopo wilaya ya Ikungi Mkoani Singida.

Amesema historia ya ujenzi wa mgodi huo, kwa miaka mitano yote iliyopita Mgodi wa Shanta ndio mgodi wa Kati mpya uliojengwa hapa Nchini.

Akizungumzia kuhusu umuhimu wa Sheria ya Local content amesema kuwa, katika uwekezaji inawahitaji wakubwa, wa kati na wadogo ili kufanya uchumi uwe na maana.

Kama biashara wafanye wenyeji, tulikuwa na migodi ambayo hata nyama ilitoka South Africa, lakini mgodi ambao mwaka huu tumewapa tuzo ya Local content, huu ndio mgodi ambao asilimia 100 ya walioajiriwa ni watanzania,”ameeleza Biteko.

Aidha, ameipongeza kampuni ya uchimbaji madini ya Shanta kwa kupiga hatua katika kusimamia Sheria hii ya Local content na manunuzi ya bidhaa katika migodi yao kwa asilimia kubwa ambao unategemea kuanza shughuli za uzalishaji wa dhahabu Mwezi Novemba 2022.

Naye, Meneja Mkuu Mahusiano ya Serikali wa mgodi wa Shanta, Philibert Rweyemamu amemueleza Waziri Biteko kuwa, wanashirikiana na uongozi wa Wilaya na Mkoa katika kutoa kipaumbele katika shughuli za maendeleo. Amesema wananchi wa Ikungi na Singida kwa ujumla wanapata ajira mbalimbali zinazotolewa na mgodi huo pamoja na manunuzi ya bidhaa mbalimbali.

Pia, Meneja Mkuu Shanta Mradi wa Singida Jiten Divecha akisoma taarifa ya mgodi huo ameeleza kuwa, hadi sasa mgodi unawafanyakazi 117 sawa na asilimia 70 ambao wameajiriwa kutoka vijiji vinavyozunguka mgodi.

Tumekamilisha vyumba vya madarasa ya shule ya Sekondari Mangonyi Shanta na madawati 183,” amesema Divecha.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Singida Binilith Mahenge ameipongeza Serikali kupitia wizara ya madini kwa mageuzi makubwa katika sekta ya madini hapa nchini. Amesema mageuzi ni mengi makubwa na utunzaji wa rasilimali madini.
Previous articleTCRA KANDA YA ZIWA YAKABIDHI LESENI KITUO KIPYA CHA REDIO CHA GOLD FM KAHAMA.
Next articleRais Dkt.Mwinyi azindua Zanzibar Golden Tulip Airport Hotel

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here