Home LOCAL DKT. GWAJIMA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA MKOA WA IRINGA QUEEN SENDIGA...

DKT. GWAJIMA AFANYA MAZUNGUMZO NA MKUU WA MKOA WA IRINGA QUEEN SENDIGA JIJINI DODOMA.


Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!

DODOMA

Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Dorothy Gwajima, leo amekutana na kufanya mazungumzo na Mkuu wa Mkoa wa Iringa Mhe. Queen Sendiga Kwenye ofisi za Wizara jijini Dodoma.

Viongozi hao wamejadili mwenendo wa utoaji huduma za afya, hali ya watumishi na dawa pamoja na maboresho ya miundombinu kwenye vituo vya kutolea huduma za afya  Katika mkoa wa Iringa.

Katika kikao hicho Mkuu wa mkoa aliambatana na Katibu Tawala wa mkoa  Bi. Happynes Seneda.