Home LOCAL MIAKA 60 YA UHURU IDARA YA MAENDELEO YA JAMII HALMASHAURI YA JIJI...

MIAKA 60 YA UHURU IDARA YA MAENDELEO YA JAMII HALMASHAURI YA JIJI WAFANYA USAFI

Kuelekea miaka 60 ya UHURU Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam leo Novemba 26/2021 Meya wa Halmashauri hiyo Omary Kumbilamoto amezindua kampeni ya Usafi Wilaya ya Ilala zahanati ya Vingunguti (Picha na Heri Shaaban)

Afisa Maendeleo Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Georgis Assenga (Kushoto)akiwa na Mwenyekiti wa Changamka mwanamke Maria Lukas leo katika kuelekea miaka 60 ya UHURU wameshiriki uzinduzi wa Usafi Wilaya ya Ilala zahanati ya Vingunguti(PICHA NA HERI SHAABAN)

NA: HERI SHAABAN

HALMASHAURI  ya Jiji la Dar es Salaam wamezindua Usafi Wilaya ya Ilala ,kwa kushirikiana na Idara  ya Maendeleo ya Jamii Halmashauri ya jiji.

Akizindua Kampeni ya Usafi ngazi ya Wilaya ya Ilala  Meya wa Halmashauri hiyo Omary Kumbilamoto  alisema   Usafi ni jukumu letu sote kila mwananchi anatakiwa kufanya usafi katika maeneo yao kwa ajili ya kutunza mazingira.

“Leo tumezindua rasmi  Kampeni ya Usafi ngazi ya Wilaya ya Ilala kata hii ya Vingunguti  wiki hii yote ni mwendelezo wa kufanya usafi endelevu uzinduzi wa Usafi kwa Mkoa wa Dar es Salaam Desemba 04/2021 kata ya Kivukoni Wilaya ya Ilala mgeni rasmi Mkuu wa Mkoa Dar es salaam Amos Makala “ alisema Kumbilamoto.

Meya Kumbilamoto amewataka wananchi kujenga tabia ya kuwa wasafi katika maeneo yao kwa kusafisha mazingira na kufanya usafi kila siku .

Akizungumzia mikopo ya vikundi alisema halmashauri tayari wameshatoa zaidi ya Shilingi bilioni 6 vikundi vimekopa na mikopo mingine wanatarajia kutoa Mwisho wa Novemba mwaka huu katika Maonesho pale Viwanja vya Mnazi Mmoja .

Kwa upande wake Afisa Maendeleo Dawati la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Georgis Asenga, alisema katika madhimisho ya miaka 60 ya UHURU Idara ya Maendeo ya Jamii wanashiriki usafi na wananchi  kwani usafi ni afya tujilinde katika maeneo yetu kwa kushiriki usafi.

Asenga alisema katika kampeni hiyo ya usafi wamefanya na vikundi mbalimbali vya kijamii,TASAF,Wajane wa Vingunguti na Changamka Mwanamke .

Mganga Mfawidhi Zahanati ya  Vingunguti Chiku Simba alisema zahanati ya Vingunguti inatoa huduma bora kwa wananchi wa eneo hilo ikiwemo huduma za mama na Mtoto.

Aidha Daktari Chiku alisema pia katika Zahanati hiyo wanatoa chanjo ya COVID kwa wananchi wote asubuhi mpaka jioni.

MWISHO.

Previous articleJAJI WARIOBA AONGOZA MAHAFALI YA 38 YA CHUO KIKUU CHA SOKOINE CHA KILIMO SUA MOROGORO
Next articleTANZANIA YACHAPWA 1-0 NA UGANDA Canaf
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here