Home LOCAL MKURUGENZI MKUU TANESCO AAGIZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA UMEME MGODI...

MKURUGENZI MKUU TANESCO AAGIZA USIMAMIZI MZURI WA MRADI WA UMEME MGODI WA DHAHABU GGM GEITA.

Na: Costantine James, Geita.

Mkurugenzi mtendaji wa shilika la umeme nchini (TANESCO)  Maharage Chande amemtaka meneja wa Tanesco mkoa wa Geita kusimamia Vyema mradi wa umeme katika mradi wa umeme kwenye mgodi wa dhahabu wa GGM ambao leo February 21 Tanesco imesai mkataba wa kuuziana umeme na na mdogi huo.

Akizungumza katika hafla ya  kusaini mktaba na mgoodi wa GGM Mkurugenzi mtendaji wa shirika la umeme nchini Maharage Chande amesema mkataba huo utaliwezesha shirika la umeme nchini Tanesco kupata bilioni 5 kwa  kila menzi.

Maharage amesema Mkurugenzi wa Tanesco pamoja na viongozi mbali mbali wa Tanesco mkoa wa Geita wanatakiwa kusimamia vyema mradi huo kwani serikali itapata mapato makubwa zaidi kutokana na mapato yatakayo tolewa na mgodi wa dhahabu GGM ambayo yataiwezesha serikali kutekeleza miradi mbali mbali ya kimaendeleo.

“Sisi sote wafanyakazi wa Tanesco injinia atakae tuangusha hapa lazima turuke naye kwa sababu anatukosesha bilioni 5. Kwa sababu umeme huu utaongeza ufanisi wa kazi zo GGM kwa maana watakuwa wanapunguza gharama katika shughuli zao” Ameaema Maharage Chande mkurugenzi mtendaji shirika la umeme nchini Tanesco.

Makamu wa Rais wa mgodi wa GGM Saimoni Shayo amesema mgodi huo kwa miaka 20 ambayo wamewekeza nchini Tanzania wamekuwa wakitumia umeme wa kazalisha kwa mafuta.

Shayo amesema licha ya umeme wanaotumia mgodini hapo ambao wanazalisha kutokana na mafuta ambayo yanamsamaha wa kodi lakini bado gharama ya kuzalisha umeme ni kubwa kuliko umeme watakao upata kutoka shirika la umeme nchini Tanesco.

“Kwetu hii inamanisha kwamba tunapunguza gharama za uzalishaji kwa maana ya kwamba gharama yetu ya kuzalisha umeme itapungua lakini zaisi tunaangalia matumizi ya kifedha tunapunguza gharama ya mafuta kama tunavyo fahamu dunia sasa inahama kwenye matumizi ya kutumia mafuta ambayoyanazalisha hewa ukaa kwenda kwenye matuzi ya nishati” Amesema Saimon Shayo makamu wa Rais GGM

Previous articlePATA HABARI KATIKA MAGAZETI YA LEO J.PILI FEBRUARI 20-2022
Next articleIODT YAWANOA WAKUKURUGEZI KUTOKA TAASISI ZA SERIKALI NA BINAFSI JUU YA MASUALA YA UONGOZI
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here