Home LOCAL MAJALIWA AWASILI SHELISHELI KUMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA UAPISHO WA RAIS MTEULE DKT....

MAJALIWA AWASILI SHELISHELI KUMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA UAPISHO WA RAIS MTEULE DKT. PATRICK

Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Oktoba 26, 2025 amewasili Seychelles kwa ajili ya kumwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye uapisho wa Rais mteule wa sita wa nchi hiyo Dr. Patrick Herminie

Tume ya Uchaguzi ya Taifa ilimtangaza Mheshimiwa Dkt. Patrick Herminie wa Chama cha United Seychelles (US) kuwa mshindi baada ya kumbwaga Rais aliyekuwa madarakani, Mheshimiwa Wavel Ramkalawan wa Chama cha Linyon Demokratik Seselwa (LDS).

Mheshimiwa Dkt. Patrick Herminie alipata asilimia 52.7% ya kura, huku Rais Wavel Ramkalawan akimaliza wa pili kwa kupata 47.3% ya kura.

http://MAJALIWA AWASILI SHELISHELI KUMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA UAPISHO WA RAIS MTEULE DKT. PATRICK