Home SPORTS SIMBA IMEREJEA KILELENI, KWA KUIZABA TANZANIA PRISONS BAO 3-0

SIMBA IMEREJEA KILELENI, KWA KUIZABA TANZANIA PRISONS BAO 3-0

Simba imerejea kwenye kilele cha Ligi ya NBC kwa kufikisha alama 47 baada ya kuwazaba Wajelajela, Tanzania Prisons kwa jumla ya mabao 3-0.

Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!

Mabao ya Simba yamefungwa na Jean Ahoua, Radack Chasambi na Elie Mpanzu na kufanya ubao usomeke 3-0 mpaka dakika 90 zinamalizika.

Nyota ya Chasambi imeng’aa upya baada ya kufunga bao na kurekebisha makosa aliyoyafanya kwenye mchezo uliopita ambapo alijifunga na kusababisha timu yake itoke sare ya 1-1 dhidi ya Fountain Gate.