Home LOCAL KATIBU MKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM AKIZUNGUMZA NA WANANCHI  JIMBO LA...

KATIBU MKUU WA CHAMA CHA MAPINDUZI CCM AKIZUNGUMZA NA WANANCHI  JIMBO LA BUCHOSA

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi akizungumza na wananchi wa Jimbo la Buchosa, Halmashauri ya Buchosa, Nyehunge, leo Agosti 14, 2024, mara baada ya kuwasili na kupokelewa Mkoa wa Mwanza, kuanza ziara ya siku 2 ya kikazi mkoani humo, akitokea Mkoa wa Geita.

Katika ziara hiyo, Katibu Mkuu Balozi Nchimbi ameambatana na Wajumbe wa Kamati Kuu ya CCM, Ndugu Issa Haji Usi Gavu, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM Taifa – Oganaizesheni, Ndugu Amos Gabriel Makalla, Katibu wa NEC – Itikadi, Uenezi na Mafunzo na Ndugu Rabia Hamid Abdalla, Katibu wa NEC – Siasa na Uhusiano wa Kimataifa.

Malengo ya ziara hiyo ya Katibu Mkuu wa CCM ni pamoja na kukagua utekelezaji wa Ilani ya CCM ya 2020 – 2024, kukagua na kuhamasisha uhai wa CCM, pamoja na kuzungumza na kuwasikiliza wananchi.

Previous articleMRADI WA 711 KAWE KUZALIWA UPYA: HATUA JASIRI YA NHC KUTIMIZA NDOTO ZA MAKAZI
Next articleDKT JAFO: KILA MKOA KUANZISHA VIWANDA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here