Home LOCAL BRELA YAWASHIKA MKONO WATOTO WENYE UHITAJI – CHAKUWAMA

BRELA YAWASHIKA MKONO WATOTO WENYE UHITAJI – CHAKUWAMA

Katika kuadhimisha Siku ya Wafanyakazi Duniani maarufu kama Mei Mosi, Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), leo tarehe 01 Mei, 2024 imetembelea Kituo cha Watoto wenye uhitaji cha CHAKUWAMA kilichopo Sinza jijini Dar es Salaam kwa ajili ya kutoa msaada wa vifaa mbalimbali.

Akikabidhi msaada huo kwaniaba ya Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA, Afisa Habari Mkuu Bi. Christina Njovu alieleza kuwa Wakala imetoa msaada huo ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sera ya kurudisha kwa jamii ambapo wakala imekuwa ikiitekeleza mara kwa mara.

Baadhi ya vifaa vilivyokabidhiwa ni pamoja na vyakula vikiwemo unga, sukari,vifaa vya usafi na vifaa vya shule

Naye Mkuu wa Kituo cha CHAKUWAMA Bw. Hassan Hamis ameishukuru BRELA kwa kufika kituoni hapo kuwatembelea na kwa msaada uliotolewa ambao umewapa faraja kubwa ikizingatiwa kwamba hivi karibuni wamepatwa na janga la moto kwa kuunguliwa na bweni la kulala Watoto.

Aidha Bw. Hamis ameeleza kuwa, Kwa sasa kituo kina watoto 72 wa jinsia zote wenye umri tofauti kuanzia chini ya mwaka mmoja hadi miaka 19 na wengi wao wanasoma shule ya msingi na sekondari na kwamba changamoto zao ni nyingi hivyo ujio wa BRELA na vifaa ilivyotoa vitapunguza ukali wa baadhi changamoto zinazowakabili.

Akielezea historia ya kituo hicho Bw. Hamis.amesema kuwa, Kituo kilianza mwaka 1998 kikiwa na Watoto 5 chini ya mwanzilishi Bi. Saida Hassan kikitumia nyumba ya kupanga eneo la Mikocheni , Kituo kimesajiliwa na kinafanya kazi kwa karibu na Wizara ya maendeleo ya jamii, jinsia Watoto na makundi maalum.

Na kuongeza kuwa kituo kina watoto aliowatenga katika makundi sita wakiwemo, yatima waliopoteza wazazi wote wawili, Watoto waliopoteza mzazi mmoja, wapo waliotolewa kwenye mazingira hatarishi na wale waliofanyiwa ukatili na walio okolewa kutoka biashara haramu ya usafirishaji wa binadamu pamoja na walemavu.

Katika Watoto 72 watoto 60 wanasoma katika ngazi tofauti kuanzia chekechea, msingi, sekondari, veta na vyuo katika shule za serikali na shule binafsi za kulipia.

Aidha Bw.Hamis ameeleza kuwa moja ya changamoto wanazokabiliana nazo ni pamoja na Watoto 12 wamesimamishwa kuendelea na masomo kutona na kuathilika kiakili kulikotokana na ukatili waliofanyiwa na wengine kupata magonjwa na hivyo wanaendelea na matibabu.

Mbali ya kutembelea kituo cha Watoto wahitaji, BRELA pia imeshiriki katika maadhimisho ya Siku ya Wafanyakazi Duniani iliyobebwa na kaulimbiu Nyongeza ya mishahara ni msingi wa mafao bora na kinga dhidi ya hali ngumu ya maisha

Previous articleMEI MOSI NI SIKU YA TAFAKURI KWA WATUMISHI-MAJALIWA
Next articleWAFANYAKAZI KUWENI NA MATUMAINI, RAIS ATASEMA JAMBO LAKE HIVI KARIBUNI – Dkt. MPANGO 
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here