Home LOCAL MKATABA BAINA YA NHIF NA APHFAT HAUJAVUNJWA – Dkt. SAGWARE

MKATABA BAINA YA NHIF NA APHFAT HAUJAVUNJWA – Dkt. SAGWARE


Mwenyekiti wa Kamati ya kupitia kitita cha mafao cha NHIF 2023 Dkt. Baghayo Saqware akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 29,2024 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.


Mwenyekiti wa Kamati ya kupitia kitita cha mafao cha NHIF 2023 Dkt. Baghayo Saqware akisisitiza jambo wakati akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 29,2024 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam.

Mwenyekiti wa Kamati ya kupitia kitita cha mafao cha NHIF 2023 Dkt. Baghayo Saqware akizungumza na waandishi wa habari leo Februari 29,2024 katika ukumbi wa Mikutano wa Kimataifa wa Mwalimu Julius Nyerere Jijini Dar es Salaam

MWENYEKITI wa Kamati ya kupitia kitita cha mafao cha NHIF 2023 Dkt. Baghayo Saqware amesema maamuzi ya ujio wa Kitita hicho ni matokeo ya makubaliano ya pande zote ambazo ni watoa huduma binafsi za Afya na BAKWATA kwa maslahi ya serikali na sekta binafsi.

Akizungumza leo Februari 29,2024 Jijini Dar es Salaam, Dkt Saqware amesema hakuna atakayekosa huduma ya matibabu kwa kuwa mkataba baina ya mfuko na watoa huduma za afya wa sekta binafsi (APHTA) haujavunjwa.

“Kamati ilikuwa huru kumsikiliza kila mtu, tulikubaliana kwa pamoja na tuliamua kitita kianze kutumika kwa faida ya nchi na taasisi zetu.

“Kwahiyo tunapenda kutoa msimamo wa kitaalam kwamba Wizara kupitia NHIF iendelee na utekelezaji wa kitita cha mafao kilichoboreshwa cha NHIF cha mwaka 2023 kama ilivyoshauriwa na kamati,” amesema Dk Saqware.

Aidha amesema kuwa mapendekezo ya kamati ya wataalam ni pamoja na kuanza kutumika kwa kitita cha mafao cha mwaka 2023 pamoja na maboresho yaliyopendekezwa na kamati katika sehemu ya ada ya ushauri na kumuona daktari, huduma za dawa, upasuaji na vipimo.

Sambamba na hilo amesema Kitita kinachotumika hivi sasa kilifanyiwa maboresho kwa mara ya mwisho mwaka 2016 hivyo Mfuko umelazimika kufanya mapitio katika Kitita hicho ili kwenda sambamba na mahitaji yaliyopo na hali halisi ya utoaji wa huduma za afya nchini.

Previous articleRAIS SAMIA ATANGAZA KIFO CHA RAIS MSTAAFU MZEE ALI HASSAN MWINYI IKULU DAR ES SALAAM 
Next articleWAFANYA BIASHARA WAKUMBUSHWA KUHUSU DHANA YA WAMILIKI MANUFAA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here