Home LOCAL WATUMISHI WA UMMA WAASWA KUTOKUWA NA HOFU NA MFUMO MPYA WA TATHIMINI...

WATUMISHI WA UMMA WAASWA KUTOKUWA NA HOFU NA MFUMO MPYA WA TATHIMINI  YA WATUMISHI.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akizungumza  leo wakati wa ufungaji wa mafunzo ya siku tatu kwa watumishi wa umma kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Shirika la Masoko Kariakoo na Bodi ya Sukari Tanzania yaliyofanyika MOI.

Na Lusungu Helela-Dar es Salaam

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete amesema Mfumo wa Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma (HRA) hauna lengo la kumuondoa kazini ama kuwaonea watumishi wa umma hivyo hawana sababu ya kuuhofia mfumo huo.

Mhe. Kikwete amebainisha hayo  wakati wa ufungaji wa mafunzo ya siku tatu kwa watumishi wa umma kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Shirika la Masoko Kariakoo na Bodi ya Sukari Tanzania yaliyofanyika MOI.

Amesema lengo la mfumo huo ni kuiwezesha kupima utendaji wa watumishi wake kwa njia rahisi na kuongeza ufanisi wenye tija kazini.

“Mfumo huu  hauna lengo la kukomoa watu, tunatakuwa na utumishi wa umma unaotimiza majukumu, utawezesha kupamga utumishi wenye tija, huna sababu ya kuhofia” amesema Mhe: Kikwete

Amesema mifumo hiyo inakwenda kuonesha wapi kwenye mapungufu ili paweze kuboreshwa

Aidha aliipongeza MOI kwa kutoa huduma bora kwa Watanzania na kuitaka kuendelea na kasi hiyo kwa maslahi ya umma.

“MOI inaendelea kuwa bora hii yote ni juhudi zako Profesa Makubi na timu yako, hongera sana, tunahitaji utumishi wenye tija” amesema

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Prof. Abel Makubi akimkaribisha Naibu Waziri huyo alimpongeza kwa kuitembelea MOI mara kwa mara na kwamba hatua hiyo inaongeza ari kwa watumishi kufanya kazi kwa umahiri.

Mkurugenzi wa Uendelezaji Taasisi, Naolasci Kipanda ambaye pia ni Mwezeshaji wa Mafunzo ya Mfumo wa Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma (HRA) Nestory Kipanga akizungumza kabla ya kumkaribisha  Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora,Mhe.Ridhiwani Kikwete leo wakati wa ufungaji wa mafunzo ya siku tatu kwa watumishi wa umma kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Shirika la Masoko Kariakoo na Bodi ya Sukari Tanzania yaliyofanyika MOI.

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa ameongozana na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Prof. Abel Makubi wakati akitembelea Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) mara baada ya kufungua mafunzo kwa watumishi wa umma

Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Prof. Abel Makubi akizungumza  leo wakati wa ufungaji wa mafunzo ya siku tatu kwa watumishi wa umma kutoka Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) Shirika la Masoko Kariakoo na Bodi ya Sukari Tanzania yaliyofanyika MOI.

Sehemu ya watumishi wa MOI Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwetewakati akizungumza nao katika ufungaji wa mafunzo ya Mfumo wa Mahitaji ya Rasilimaliwatu katika Utumishi wa Umma (HRA)

Naibu Waziri Ofisi ya Rais, Menejimenti ya  Utumishi wa Umma na Utawala Bora Mhe. Ridhiwani Kikwete akiwa  na Mkurugenzi Mtendaji wa MOI Prof. Abel Makubi wakati akitembelea Taasisi ya Tiba ya Mifupa na Ubongo Muhimbili (MOI) akiangalia baadhi ya mashine za kisasa za mionzi zilizopo katika Taasisi hiyo.

 

Previous articleARDHI SACCOS YATAKIWA KUONGEZA UBUNIFU KULETA MAENDELEO
Next articleSERIKALI YAFUTA MASHIRIKA 4 YA UMMA, YAUNGANISHA 16

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here