Home LOCAL UONGOZI WA TEMEKE HOSPITALI WAFANYAKAZI NZURI KATIKA KUBORESHA HUDUMA

UONGOZI WA TEMEKE HOSPITALI WAFANYAKAZI NZURI KATIKA KUBORESHA HUDUMA

Dar es Salaam, Tarehe 1 Desemba 2023

Mhe. Mary Chatanda, Mwenyekiti wa Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) Taifa wa Chama cha Mapinduzi (CCM), ametoa pongezi kwa uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke (TRRH) kwa juhudi zao za kusimamia na kuboresha huduma za afya. Katika ziara yake ya leo katika hospitali hiyo, Mhe. Chatanda ameelezea kufurahishwa kwake na maendeleo na ubora wa kazi inayofanywa na wataalamu na uongozi wa hospitali.

Akizungumza mbele ya waandishi wa habari, Mhe. Chatanda alisisitiza umuhimu wa kazi inayofanywa na wataalamu na uongozi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa Temeke, akielezea jinsi wanavyoshirikiana kwa uaminifu na kwa uangalifu mkubwa katika kusimamia na kuboresha majengo ya hospitali. Aliongeza kuwa ubora wa huduma unatokana na juhudi zinazofanywa na wafanyakazi wote kwa pamoja.

Ziara hiyo ilihusisha pia Naibu Mwenyekiti wa UWT, Mhe. Zainab Shomari, pamoja na Katibu Mkuu wa UWT, Mhe. Jokate Mwegelo, na viongozi wengine wa UWT. Walipata fursa ya kutembelea Wodi za kina mama waliojifungua na wale wanaosubiri kujifungua, ambapo walishuhudia juhudi za hospitali katika kutoa huduma bora za afya kwa wananchi.

Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hospitali hiyo, Dkt. Joseph Kimaro, alielezea mikakati mbalimbali inayofanywa na hospitali kuboresha huduma za afya. Alisisitiza kuwa hospitali inaendelea kukua na kueleza kuhusu ongezeko la idadi ya madaktari bingwa. Pia, alitangaza mipango ya kuanzisha miradi kama vile wa usafishaji damu (Dialysis), ambao unatarajiwa kukamilika kwa ushirikiano na mdau wao muhimu, TPA.

 

Previous articleMAANDALIZI KUELEKEA SIKU YA UKIMWI DUNIANI YAKAMILIKA
Next articleKINANA KERO ZA UMEME NA MAFUTA ZAJADILIWA KATIKA KIKAO CHA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here