Home LOCAL MEJA JENERALI MBUGE “MIKOA IANZISHE TIMU YA WATAALAM YA KUKABILIANA NA  MAAFA”

MEJA JENERALI MBUGE “MIKOA IANZISHE TIMU YA WATAALAM YA KUKABILIANA NA  MAAFA”

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Meja Jenerali Charles Mbuge akifungua Kikao kazi cha Kuweka Mkakati wa Kuanzisha Timu ya Wataalam ya Kukabiliana na Maafa  Mkoa wa Dodoma (Dodoma Mult Agency Emergency Response Team – DoMAERT) kilichofanyika  Jijini Dodoma.

Baadhi ya Wajumbe wa  Kamati ya Wataalam ya Usimamizi wa Maafa kutoka  Halmashauri  ya Jiji la Dodoma na Halmashauri ya Wilaya ya Chamwino mkoani Dodoma wakifuatilia kikao hicho

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Meja Jenerali Charles Mbuge (wa tano kushoto) akiwa katika picha ya pamoja  na baadhi ya Wajumbe wa  Kamati ya Wataalam ya Usimamizi wa Maafa baada ya  Kikao kazi cha Kuweka Mkakati wa Kuanzisha Timu ya Wataalam  ya Kukabiliana na Maafa  Mkoa wa Dodoma (Dodoma Mult Agency Emergency Response Team – DoMAERT) kilichofanyika  Jijini Dodoma.

Na: Mwandishi wetu- Dodoma

Mkurugenzi wa Idara ya Menejimenti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu Meja Jenerali Charles Mbuge  amewataka Wataalam kuanzisha Timu Mtambuka ya Wataalam ya Kukabiliana wa Maafa kila Mkoa ambayo itarahisisha  mawasiliano ndani ya Mkoa wakati wa kukabiliana na dhahrura.

Meja Jenerali Mbuge ameyasema hayo wakati akifungua Kikao Kazi cha Kuweka Mkakati wa Kuanzisha Timu ya Wataalam ya Kukabilianana Maafa  Mkoa wa Dodoma (Dodoma Mult Agency Emergency Response Team – DoMAERT) kilichofanyika  Jijini Dodoma.

Amesema uwepo wa timu hiyo pia itasaidia kuunganisha nguvu kwa wadau waliopo ndani ya Mkoa na kuweza kutumia rasilimali zilizopo kuhakikisha maafa yanakabiliwa na wananchi kuwa katika mazingira salama.

“Nchi yetu imekuwa ikipata maafa mara kwa mara ambayo uratibu wake unahitaji kila Mkoa kuwa na Timu Mtambuka ya Wataalam ya Kukabiliana wa Maafa kwa mujibu wa Sheria ya Usimamizi ya Maafa Na. 6 ya mwaka 2022 na kanuni zake hivyo uundwaji wa timu hizo ni muhimu kwa usalama wa wananchi na mali zao,” Amesema Meja Jenerali Mbuge.

Pia Mkurugenzi huyo  amewasisitiza  washiriki kupitia kikao kazi hicho kuhakikisha kila mmoja  kwa nafasi yake anafahamu jukumu lake na  kulitekeleza kikamilifu pamoja na  tayari kwa ajili ya kukabiliana na maafa ndani ya Mkoa.

Katika hatua nyingine ameeleza Meja Jenerali Mbuge kwamba Idara ya Menejimeti ya Maafa Ofisi ya Waziri Mkuu  imeendelea kuchukua hatua za kupunguza madhara kwa kuhakikisha usimamizi na uratibu wa maafa na huduma za dharura zinatolewa kwa wakati kwa kuzingatia mipango, miongozo na mikakati ya kitaifa na kisekta.

“Idara ya Menejimenti ya Maafa kwa kuzingatia Sera ya Taifa ya Usimamizi wa Maafa ya Mwaka 2004 na Sheria ya Usimamizi wa Maafa, Na. 6 ya mwaka 2022 inaratibu na kusimamia masuala ya maafa nchini,”Amebainisha Mkurugenzi huyo.

Aidha Mkurugenzi huyo akawahimiza wananchi kushirikiana na Serikali pamoja na wadau wa maendeleo ili kuhakikisha malengo ya mapambano dhidi ya maafa yanafaikiwa kama iliyokusudiwa.

MWISHO

Previous articleBALOZI WA UHOLANZI AMPONGEZA RAIS SAMIA KUIMARISHA UTENDAJI KAZI WA VYOMBO VYA HABARI NCHINI
Next articleWAZIRI MKUU ATEMBELEA MAONESHO YA SIKU YA KIFUA KIKUU DUNIANI KITAIFA SIMIYU
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here