Home KIDSNEWS MEYA KUMBILAMOTO ATAKA FAHARI WAUNGWE MKONO KUKOMESHA UKATILI KWA WATOTO

MEYA KUMBILAMOTO ATAKA FAHARI WAUNGWE MKONO KUKOMESHA UKATILI KWA WATOTO

Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto akikabidhi kadi za Bima ya Afya Kwa watoto Maalum ambao wapo katika Mazingira Magumu ,Leo Juni 15/2022 Ukonga katika Madhimisho ya siku ya mtoto wa Afrika Dunia, Kadi za Bima ya Afya zimetolewa na Fahari Day Care Kwa ajili ya kusaidia matibabu,(Kulia) Mkurugenzi wa Fahari Day Care Neema Mchau (PICHA NA HERI SHABAN)

NA: HERI SHAABAN

Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam, Omary Kumbilamoto, ameipongeza Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo kwa jitihada zake za kupambana na vitendo vya ukatili kwa watoto na kuwataka wadau wengine kuiunga mkono.

Kumbilamoto aliyasema hayo katika  wakati wa maadhimisho ya Siku ya Mtoto wa Afrika yaliyoandaliwa na taasisi ya Fahari na kufanyika katika viwanja vya Shule ya Msingi Ulongoni.

Alisema ukatili unatokea kwa sababu watu wengi hawana hofu ya Mungu na kuwataka wazazi na walezi kumrudia Mungu.

“Kama ingekuwa waislam wanafuata maandiko, wakristo wanafuata maandiko ukatili usingetokea katika taifa letu kwa sababu maelekezo ya dini zote yanakataa kuwafanyia watoto ukatili,” alisema Kumbilamoto.

Kwa upande wake Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya Fahari Tuamke Maendeleo, Neema Mchau, alisema katika kuadhimisha siku hiyo waliguswa pia kutoa msaada kwa watoto 100 wanaoishi kwenye mazingira magumu wanaosoma katika Shule za Msingi Ushindi na Ulongoni.

Previous articleWAZIRI MULAMULA AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA MAMBO YA NJE WA FINLAND
Next articleBILIONI 6 ZIMETENGWA KUBORESHA MIUNDOMBUNU YA KUTOLEA HUDUMA ZA AFYA HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA SHINYANGA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here