Home LOCAL ILALA WAZINDUA KAMPENI YA MAZINGIRA KUPANDA MITI MILIONI 1.5

ILALA WAZINDUA KAMPENI YA MAZINGIRA KUPANDA MITI MILIONI 1.5

Mkurugenzi wa Kampuni ya Usafi Kajenjele (Kushoto ) akikabidhiwa cheti Cha pongezi na Mkuu wa Wilaya ya Ngw’ilabuzu Ludigija katika juhudi za kuisaidia Serikali kuipendezesha Wilaya llala katika Usafi Cheti hicho Cha usafi amepewa Leo katika Uzinduzi wa Mazingira Dunia Juni 02/2022 (katikati)Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Omary Kumbilamoto na Diwani wa Gerezani Fatuma Abubakar (PICHA NA HERI SHAABAN).

Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng’wilabuzu Ludigija akimkabidhi cheti Cha Pongezi Mkurugenzi wa Kampuni ya Usafi KIMWEDE Aisha Mrutu Leo Juni 02/2022 Katika Madhimisho ya siku ya Mazingira Dunia Wilayani Ilala Kampuni ya KIMWEDE Moja ya Kampuni ya Usafi inaunga mkono juhudi za Serikali katika kuipendezesha Wilaya llala (katikati)Meya wa Halmashauri hiyo Omary Kumbilamoto (Picha na HERI SHAABAN)


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng’wilabuzu Ndatwa Ludigija akimkabidhi cheti Cha pongezi Mkurugenzi wa Kampuni ya Usafi SATEKI SAUDA URASA katika uzinduzi wa Siku ya MAZINGIRA Duniani Leo Juni 02/2022 , Kampuni ya SATEKI Moja ya Kampuni ya Usafi Wilaya ya Ilala inaunga mkono juhudi za Serikali katika kuipendezesha Ilala (katikati)Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto na Diwani wa Kata Gerezani Fatuma Abubakar ( PICHA NA HERI SHABAN).


Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng’wilabuzu Ndata LUDIGIJA akimkabidhi cheti Cha Pongezi Katibu wa Jumuiya ya Wazazi Wilaya ya Ilala Mtiti Mbasa katika uzinduzi wa Siku ya MAZINGIRA Duniani Leo Juni 02/2022 madhimisho yanayofanyika Juni Kila Mwaka , Jumuiya ya Wazazi Ilala imeweza kuunga mkono juhudi za Serikali katika utunzaji MAZINGIRA (katikati)Mkurugenzi wa HALMASHAURI ya Jiji Dar es Salaam Jumanne Shauri na Meya wa HALMASHAURI hiyo Omary Kumbilamoto (PICHA NA HERI SHABAN.

NA: HERI SHAABAN (ILALA), Herishaban@gmail.com

WILAYA YA ILALA inatarajia kupanda miti milioni 1.5 kwa ajili ya kampeni ya utunzaji Mazingira na kuhifadhi vyanzo vya maji .

Hayo yalisemwa na Mkuu wa Wilaya ya Ilala Ng’wilabuzu Ndatwa Ludigija katika uzinduzi wa siku ya MAZINGIRA Duniani ambapo Wilaya ya Ilala imezindua kwa kufanya usafi na kupanda miti ndani ya Wilaya llala.

Uzinduzi huo wa wiki ya Mazingira Wilaya ya Ilala ulizinduliwa Dar es Salaam Juni 02/2022 katika Kata ya Gerezani Kariakoo ambapo wadau wa Mazingira na Wakandarasi wa Kampuni za uzoaji taka walipongezwa sambamba na Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam kwa kazi nzuri ya kulipendezesha Jiji hilo katika Mazingira ya usafi na kuifanya Wilaya ya Ilala kupendeza.

“Kampeni yetu ya utunzaji Mazingira katika Wilaya ya Ilala tunatarajia kupanda miti milioni 1.5 naomba Wananchi wote tupande miti katika maeneo yetu hii ni kampeni endelevu kwa kila Kata kila kaya na kila mmoja wetu aone fahari kupanda miti ili kukabiliana na mabadiliko ya Tabia ya nchi” alisema Ng’wilabuzu.

Mkuu wa Wilaya Ng’wilabuzu amewataka Wananchi wa Wilaya ya Ilala pia kupanda miti ya vivuli pamoja na miti ya matunda katika maeneo yao.

Wakati huo huo Ludigija aliwapongeza Wakandarasi wa Kampuni za usafi ambao wanalipendezesha Jiji hilo kwa usafi na baadhi ya kampuni za usafi zilipewa pongezi kwa kutambua mchango wao kampuni hizo ni KAJENJELE,KIMWEDE na SATEKI za jijini Dar Salaam.

Alisema Jiji la Dar es Salaam limeshika nafasi ya sita kwa usafi Barani Afrika, ni Jiji Bora sura ya nchi yetu TANZANIA inabebwa na Jiji hilo hususani Wilaya ya Ilala .

Katika hatua nyingine Ludigija amewataka Waendesha Bodaboda na Bajaj wa Wilaya ya Ilala kufuata taratibu katika vituo vyao vya kazi walivyopangiwa hili Halmashauri ya Jiji Dar es Salaam iweze kupendeza .

Pia aliwataka Waendesha Bodaboda na Bajaj kufuata kanuni za usafi katika vituo vyao walivyopangiwa kwa kufanya usafi kila wakati na vyombo vya usafiri ikiwemo Daladala kufunga vifaa Maalum vya kuifadhia taka taka.

Kwa upande wake Meya wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam Omary Kumbilamoto alisema Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam inajivunia kwa usafi kwa Sasa miaka sita Ilala amna ugonjwa wa kipindupindu ni juhudi kubwa zilizofanywa na Watendaji wa Wilaya hiyo pamoja na MAAFISA Afya katika kitunza Mazingira.

Afisa Mazingira wa Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam RAJABU NGODA alisema katika wiki ya Madhimisho ya Mazingira Duniani kuanzia Juni Mosi mpaka Juni tano Halmashauri ya Jiji hilo imejipanga kutoa elimu ya usafi wa Mazingira katika shule Kumi pamoja na Kampeni endelevu ya Upandaji miti ya matunda na kivuli.

Mwisho.

Previous articlePOLISI GEITA YAWANASA WATU WATATU KWA TUHUMA ZA UTAPELI WAKIJIFANYA MAAFISA WA SERIKALI.
Next articleLIST OF POSTGRADUATE DEGREE PROGRAMMES JULY, 2022
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here