Home SPORTS POLISI YAICHAPA AZAM FC 2-1

POLISI YAICHAPA AZAM FC 2-1

Mwandishi wetu MOSHI.

POLISI Tanzania yaibuka na ushindi  wa 2-1 dhidi ya Azam FC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa Ushirika mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Katika mtanange huo mabao ya Polisi leo yamefungwa na Kassim Shaaban dakika ya 23 na Adam Adam dakika ya 40, wakati la Azam FC limefungwa na Iddi Suleiman ‘Nado’.

Ni ushindi wa pili kwa polisi Tanzania baada ya kuichapa KMC 2-0 kwenye mechi ya kwanza Karatu, wakati Azam FC wanafikisha mechi mbili bila ushindi, kufuatia kutoa sare ya 1-1 na Coastal Union Jijini Tanga.

Mechi nyingine ya Ligi Kuu leo, Coastal Union imetoa sare ya pili mfululizo nyumbani, 0-0 na KMC Uwanja wa Mkwawani, Tanga

Previous articleBUMBULI: YANGA IPO IMARA KUNYAKUA POINTI TATU DHIDI YA GEITA.
Next articleTWIGA STARS YATINGA NUSU FAINALI COSAFA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here