Home SPORTS SIMBA SC YATANGAZA TAREHE YA KUZINDUA JEZI ZAO MPYA.

SIMBA SC YATANGAZA TAREHE YA KUZINDUA JEZI ZAO MPYA.

Kaimu Msemaji wa timu ta Simba Ezekiel Kamwaga akizungumza na waandishi wa habari juu ya ujio wa jezi mya za timu hiyo unaotarajiwa kufanyika Septemba 4,2021 Jijini Dar es Salaam. (PICHA NA: HUGHES DUGILO)

Mfanyabiashara maarufu wa Mavazi anaetengeneza na kusambaza jezi za timu ya Simba Fredy Vunjabei akizungumza kwenye mkutano namna alivyojipanga kimauzo na kuwafikia mashabiki mbalimbali wa timu hiyo popote nchini na nje ya nchi. PICHA NA: HUGHES DUGILO)

DAR ES SALAAM.
Klabu ya Wekundu wa Msimbazi Simba SC leo Septemba 1 imetangazatarehe rasmi ambayo jezi zao mpya zitazinduliwa kwaajili ya msimu wa ligi kuu Tanzania Bara inayotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Ezekiel Kamwaga ni Kaimu Msemaji wa Klabu ya Simba anafafanua kuwa Klabu hiyo ya Msimbazi ya Jijini Dar es Salaam iliingia makubaliano na Fredy Vunjabei ya kuuza na kusambaza jezi za Simba kwa mkataba wa Sh. Bilion mbili na kwamba katika siku hiyo ya Septemba 4 kutafanyika uzinduzi rasmi.

“Kabla ya Klabu ya Simba kuingia mkataba na Vunja Bei tulikuwa na Umbro na tulikuwa na mafanikio makubwa na Simba ni sehemu ya mafanikio.Tunafahamu biashara ya jezi na vifaa vya michezo ndio biashara kubwa duniani ,zaidi ya trilioni 84 zinapatikana katika biashara ya vifaa vya michezo na jezi,”amesema Kamwaga.

kwa upande wake mfanyabiashara Fred Vunja Bei amesema kuwa wao kama wasambazaji wa jezi hizo watahakikisha wanaoyesha uaminifu mkubwa kwenye zoezi zima nakwamba kila mwanasimba ataweza kupata jezi hiyo popote pale alipo ndani na nje ya nchi.


“Simba imetuamini na sisi tutaonesha uaminifu, hakuna jezi ambayo imetengezwa ikavuja hadi sasa.Kwenye mitandao zimewekwa jezi nyinyi lakini ukweli jezi yetu haijavuja mpaka sasa.Jezi zetu za msimu huu zitazinduliwa Septemba 4 mwaka huu.

“Tutakuwa na wadau wa michezo kutoka sehemu mbalinbali, tumejipanga, tunajua ukubwa wa Simba, hivyo uzinduzi wetu tutaufanya kwa ukubwa wa Simba, kutakuwa na uzinduzi wa aina mbili, Septemba 4 watazindua kuanzia saa 11 hadi saa tatu usiku,na itakuwa live Azam TV, na uzinduzi wa aina ya pili utakuwa wa mtandaoni kwa ajili ya kuuza jezi mtandaoni,”amesema Fred Vunja Bei.
Mwisho.

Previous articleRC MAKALA AWATAKA VIONGOZI WA WILAYA UBUNGO KUSHUGHULIKIA MATAPELI WA ARDHI
Next articleMSANII WA BONGO FLEVA WHOZU AZINDUA WIMBO MAALUM WA SIMBA SC
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here