Home LOCAL RC SENYAMULE ATOA MAAGIZO UKARABATI STENDI YA MABASI GEITA.

RC SENYAMULE ATOA MAAGIZO UKARABATI STENDI YA MABASI GEITA.

Na: Paul Zahor, GEITA, RS.

Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhe. Rosemary Senyamule ameiagiza Halmashauri ya Mji Geita ndani ya siku saba kuanza kufanya ukarabati wa Stendi ya Mabasi Mjini Geita ili iwe na Mazingira rafiki kwa watumiaji ikiwa ni pamoja na Maegesho, vifaa vya kuwekea takataka na Mifereji ya maji  kwa kuzingatia wakati wa masika unakaribia.

Mhe. Mkuu wa Mkoa ameyasema hayo Septemba 13, 2021 wakati alipozuru kwenye Stendi hiyo kusikiliza kero za wananchi na ndipo alipofanya Mkutano na wafanyabiashara na wasafirishaji kwenye Stendi hiyo.

“Umuhimu wa hii Stendi haubadiriki, hata kama baada ya ujenzi wa Stendi mpya aidha Stendi hii itakua ya magari makubwa au madogo bado hii ni Stendi na itaendelea kutumika, hivyo basi ni lazima tuiboreshe Stendi hii. Amesisitiza.

Vilevile, Mhe. Mkuu wa Mkoa ameagiza kuanza haraka kwa taratibu za Ujenzi wa Stendi mpya kama vikao na kutafuta mkandarasi ili ijengwe mapema iwezekanavyo kutokana na umuhimu wake kwa wakati huu.

“Ndugu viongozi twendeni tukajenge Stendi Mpya kama Mhe. Rais Samia Suluhu Hassan anavyotaka Mambo yaende kwa viwango lakini kwa speed na sio kusubiri subiri.” Amesisitiza.

Aidha, Mhe. Mkuu wa Mkoa amempongeza Mhe Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwajali wananchi wa Geita na watanzania kwa ujumla kwa kuongeza bajeti kwenye Utekelezaji wa Miradi mbalimbali ambayo kwa kukamilika kwake itasaidia wananchi kupata huduma za kijamii kama Maji, Elimu, Afya, Nishati na Barabara.

“Mhe. Rais ametoa Bilioni 100 kwa ajili ya kuleta Maji kutoka kwenye ziwa Viktoria na itakapokamilika Miradi hii basi moja kwa moja  suala la maji hapa Geita itakua historia, aidha tunashukuru sana kwa Bilioni 7 alizotupatia kwenye kila jimbo Mkoani Geita kwa ajili ya kutekeleza Miradi ya Barabara kupitia Wakala wa Barabara Vijijini na Mijini (TARURA).” Amesema.

Naye Mkuu wa Wilaya ya Geita, Mhe. Simon Shimo amekemea vikali tabia ya watoto kufanya Shughuli za biashara kwenye Stendi na ametoa wito kwa Viongzi wa Stendi  kuhakikisha wanazuia suala hilo lisitokee.

Tunatarajia kuhama hapa na Stendi mpya itakuwepo eneo la Magogo, Ujenzi unaanza hivi karibuni lakini pamoja na hilo bado tunakuja kuweka ‘Crush dust’ hapa ili kuboresha eneo hili.” Rashid Mohamedi Kaimu Mkurugenzi.

Previous articleHABARI KUU MAGAZETI YA LEO J.NNE SEPTEMBA 14-2021
Next articleYANGA YAAHIDI KUPINDUA MEZA NIGERIA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here