Home BUSINESS WAZIRI MULAMULA AITAKA STAMICO KUUTANGAZA MKAA MBADALA WA MAKAA YA MAWE.

WAZIRI MULAMULA AITAKA STAMICO KUUTANGAZA MKAA MBADALA WA MAKAA YA MAWE.

WAZIRI wa  Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki liberata Mulamula (wa kwanza kulia) Akitia saini kitabu cha wageni katika la STAMICO alipofika kwenye Banda lao kujionea shughuli mbalimbali zinazofanywa na Shirika hilo. (wa kwanza kushoto) ni Afisa Uhusiano wa STAMICO Bibiana Ndumbaro (Kutoka Kushoto kwa Afisa Uhusiano) ni Mamisi waliopo ndani ya Banda la STAMICO ni warembo ambao wapo maalum kwa ajili ya kutangaza na  kutoa elimu kuhusu mkaa mbadala wa Makaa ya mawe Rafiki briquette.
WAZIRI wa  Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki liberata Mulamula ( kulia mwenye kitenge) Akizungumza na Afisa Uhusiano wa STAMICO Bibiana Ndumbaro (kushoto) katika Banda la Shirika hilo kwenye maonesho ya Sabasaba Jijini Dar es Salaam.

WAZIRI wa  Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki liberata Mulamula (wa pili kulia)  mara baada ya kumaliza ziara yake katika Banda hilo.

Na: Mwandishi wetu, DAR ES SALAAM

WAZIRI wa  Mambo ya nje na ushirikiano wa Afrika Mashariki liberata Mulamula emetoa maelekezo kwa Shirika la Madini nchini STAMICO kujitangaza zaidi ili watanzania na wadau mbalimbali waweze kunufaika na mradi huo wa makaa mbadala makaa ya mawe.

Amesema niwakati mzuri Kwa Shirika la Stamico kujipanga hususani kupitia maonyesho hayo ili Wananchi wajuwe rasimali ambazo zipo katika nchi yao hasa Kwa kupitia wizara ya Madini chini ya Stamico.

Waziri Mulamula ameyasema hayo leo kwenye maonyesho ya 45 ya kimataifa  yanayoendelea kwenye viwanja vya maonyesho ya Sabasaba Wilayani Temeke ambalo wamepongeza mradi wa mkaa mbala wa makaa ya mawe ambao unazalishwa kwenye mgodi wa kiwila Uliochini ya Shirika hilo

Amesema kuwa  amependa bidhaa hiyo ya mkaa aa makaa ya mawe kuhalakisha kwani  hata yeye kwenye eneo lake wanahitaji bidhaa hiyo Kwa ajijili ya matumizi ya majumbani.,

“Harakisheni bidhaa hii ili iweze kutumika Kwa Wananchi  kwani wanahamu ya kuitimua na kama nilivyosema awali kwamba bidhaa hii hata kwetu Mkoani Kagera Wananchi wanahitaji sana.” Amesema Waziri Mulamula 

Ameongeza kuwa amefurahishwa  na muonekane wa Banda la Shirika hilo ukilinganisha na nyakati zingine zote na hiyo anaonyesha namna gani wamejipanga hususani katika maonyesho ya Mwaka huu.

Kwaupande wake Ofisa Uhusiano wa Shirika hilo Bibiana Ndumbaro akizungumzia ujio huo wa Waziri wa mambo ya nje Mulamula amesema kuwa ameshukuru Kwa ujio wa Waziri huyo na kuwapa moyo Kwa ubunifu ambao amruona .

Pia ametoa Maelekezo Kwa Shirika hilo kuongeza kadi ya kutangaza mradi huo ili ufike mbali zaidi na watu wauelewe zaidi mradi wa makaa mbadala ambao ukikamilika utaleta tija sana Kwa Wananchi wa Tanzania na nje ya nchi.

Mwisho.
Previous articleWAZIRI MKUU ASHIRIKI IBADA YA MISA TAKATIFU YA KUSIMIKWA ASKOFU SIMONI CHIBUGA MASONDOLE, BUNDA MUSOMA
Next articleMARAGASHIMBA AJENGA OFISI YA SERIKALI YA MTAA

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here