Home BUSINESS CHUO KIKUU CHA SOKOINE (SUA) YAANZISHA SHAHADA YA KWANZA YA UFUGAJI NYUKI...

CHUO KIKUU CHA SOKOINE (SUA) YAANZISHA SHAHADA YA KWANZA YA UFUGAJI NYUKI NA UZALISHAJI ASALI.

Mhadhiri Chuo Kikuu cha Sokoine (SUA) Dk Innocent Babili akizungumza alipohojiwa na waandishi wa habari kwenye Maonesho ya 16 ya Elimu ya Juu yaliyoandaliwa na Tume ya 
Vyuo Vikuu nchini (TCU) Viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam.
 

Mhadhili msaidizi (SUA) Hekima Mliga (wa kwanza kulia) akizungumza na moja ya mwanafuzi aliyefika kwenye Banda la SUA kwenye mMaonesho ya Vyuo Vikuu Jijini Dar es Salaam. (wa pili kulia) ni Anitha Ngesi Afisa Udahili Ndaki ya Mizengo Pinda iliyopo Katavi Mkoani Rukwa.

Maafisa Udahili wa Chuo Kikuu cha Sokoine wakiendelea na zoezi la kuwadahili wanafunzi wapya waliojitokeza kuomba kujiunga na Chuo hicho katika mwaka wa masomo 2021/2022 kwenye maonesho ya Vyuo Vikuu yanayoendelea Jijini Dar es Salaam. (wa kwanza kulia ) ni Christopher Ndaga, (katikati) Petter Msumari, na (wa kwanza kushoto) ni John Lyatuu.

 DAR ES SALAAM.

Chuo Kikuu cha  Kilimo Sokoine  (SUA) kimesema kuwa  kimeanzisha shahada ya kwanza ya  usimamizi wa rasilimali za nyuki ambapo Programu hiyo ikiwa ni ya kwanza kutolewa nchini inalenga kuzalisha watalaam waliobobea kwenye ufugaji nyuki, uzalishaji wa asali na mazao yatokanayo na nyuki.

Akizungumza nawaandishi wa habari kwenye maonesho ya 16 ya Elimu ya Juu, Sayansi na Teknolojia  Jijini Dar es Salaam mhadhiri wa  chuo hicho Dk Innocent Babili amesema kuwa amesema kuwa kozi hiyo inatolewa katika kampasi ya Katavi ambako pia wanafunzi wanapata fursa ya kujifunza kwa vitendo.

“Tumeipeleka hii program Katavi kwa kuwa kuna maeneo ya kufugia nyuki na wanafunzi wataweza kujifunza kwa vitendo. Mwitikio umekuwa mzuri, vijana wengi wameonekana kuichangamkia na kwa mwaka mpya wa masomo tunatarajia kudahili wanafunzi 100.

“Kozi hii tumeianzisha kwa kusudi maalum la kutengeneza wataalam ambao watasaidia kuongeza kiasi na ubora wa asali inayozalishwa nchini ili kukidhi viwango vya kimataifa. Kama  nchi  bado hatujatumia vizuri rasilimali za misitu na nyuki, miundombinu na uwezo tulionao ni mkubwa lakini tunazalisha kidogo yani chini ya uwezo wetu,” alisema Dk Babili

Sambamba na kuzalisha watalaam katika kampasi hiyo ya Katavi pia  inatoa mafunzo ya muda mfupi kwa wakazi wa jirani na chuo hicho wanaojihusisha na ufugaji nyuki.

Kwa upande wake Afisa udahili wa chuo hicho Christopher Ndaga amesema kuwa kozi hiyo inahusisha ufugaji wa nyuki, jinsi ya kuwatunza na kuweza kuzalisha asali ya kutosha na mazao mengine yanayotokana na nyuki na kwamba kutaongeza tija kwa wafugaji nyuki na wazalishaji asali kwa ujumla na kuweza kukuza kipato na kuimalisha uchumi wao kwa ujumla.

Previous articleMKUTANO WA WATOA HUDUMA ZA MAHUDHUI NA WADAU WENGINE KATIKA KANDA YA KATI YA TCRA, DODOMA
Next articleWIKI YA AZAKI 2021 KUFANYIKA JIJINI DODOMA, WADAU WAKUTANA KUFANYA UZINDUZI RASMI DSM.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here