Home LOCAL MHE.BITEKO AWATAKA WANANCHI KULINDA MAENDELEO YA SHULE 

MHE.BITEKO AWATAKA WANANCHI KULINDA MAENDELEO YA SHULE 

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewataka wazazi na walezi nchini kutumia fursa ya miundombinu ya shule inayojengwa kwa ushirikiano wa Serikali na wafadhili kuwasomesha Watoto na hatimaye kuchochea maendeleo.

Dkt. Biteko amesema hayo wakati akizindua miundombinu ya Shule ya Sekondari ya Milles and Kimbery White iliyojengwa kwa zaidi ya shilingi Bilioni 12 Wilayani Mkinga kwa lengo la kuwawezesha Watoto wa eneo hili kujikwamua katika ya elimu.

Miundombinu imejengwa kwa gharama kubwa ni vema ikatunzwa na kuhifadhiwa ili iwe na manufaa kwa jamii na taifa kwa ujumla”.

Pia amewataka wanafunzi kutumia nafasi wanayoipata kujiendeleza kwa kujisomea na kujenga uelewa huku wakichukua tahadhari dhidi ya baadhi ya maudhui yanayopatikana katika mitandao ya kijamii kwa kufanya hivyo hawatajuta kutokana na matokeo mazuri watakayoyapata.

Kwa upande wake, Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Profesa Adolph Mkenda amesema Wizara yake imejipanga kuanzisha mafunzo ya amali ambapo shule zaidi ya 100 zitajengwa nchi nzima ili kuwawezesha wanafunzi wahitimu elimu wakiwa na ujuzi.

Amesema jitihada kubwa iliyotumika kuweka uwekezaji katika miundombinu ya shule hiyo italindwa na kuendelezwa ili kuhakikisha malengo yaliyokusudiwa.

Naye Mtendaji wa Mkuu wa ABBOTT, Robert Ford amesema ujenzi wa shule hiyo unakusudia kuwasaidia Watoto katika eneo hilo kupata elimu na ujuzi huku akiwashukuru wakazi wa eneo la Mapatano kwa ushirikiano walionesha katika kipindi chote cha utekelezaji wa mradi.

Previous articleTANECU YAANZA SAFARI YA USHIRIKA IMARA KWA KUZINDUA VIWANDA VYA KUBANGUA KOROSHO
Next articleTAARIFA YA BEI ZA UNUNUZI WA DHAHABU KUTOKA BENKI JUU YA TANZANIA (BoT)

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here