Home BUSINESS KITUO CHA TARI NDENGU KUFUFULIWA

KITUO CHA TARI NDENGU KUFUFULIWA

Kituo cha Utafiti wa Kilimo cha TARI kilichojengwa mwaka 1959 katika eneo la Ndengu, Wilayani Mbinga kwenye Mkoa wa Ruvuma kimeelekezwa kufufuliwa ili kianze shughuli za uzalishaji wa mbegu za ngano, tafiti za mbegu za mpunga na muhogo, pamoja na upimaji wa afya ya udongo.

Ameelekeza hayo Mhe. Hussein Bashe (Mb), Waziri wa Kilimo aliposimama kukikagua wakati wa ziara yake katika Wilaya za Nyasa na Mbinga tarehe 20 Septemba 2024.

Waziri Bashe ameongeza zaidi kuwa Mkurugenzi wa TARI Uyole, Dkt. Tippe ahakikishe Kituo hicho kitakufufuliwa kwa ushirikiano kati ya Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI) na Wakala wa Mbegu Bora za Kilimo (ASA) ili kuzalisha mbegu kwa wingi kusaidia wakulima wa Wilaya hizo mbili ambao wanafanya kilimo cha kahawa, mpunga, muhogo, michikichi, mahindi na mazao mengine.

Naye Dkt. Tippe ameomba Watumishi wa tatu wa Kituo hicho wapatiwe pikipiki kusaidia usafiri; ambapo ombi hilo Mhe. Waziri Bashe aliridhia na kuielekeza Wizara ya Kilimo iwapatie pikipiki tatu.

Aidha, Kampuni ya Mbolea Tanzania (TFC) nayo imeelekezwa kusaidia upatikanaji wa mbolea za ruzuku ili wakulima wa eneo hilo waweze kunufaika kama ilivyoelekezwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kuwa mbegu za ruzuku zisambazwe kwa wakulima na kwa wakati.

Previous articleSKIMU 8 ZA UMWAGILIAJI KUNUFAISHA WANANCHI WA WILAYA YA NYASA
Next articleSERIKALI KULETA MAPINDUZI TASNIA YA KAHAWA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here