Home LOCAL WANAUME ACHENI KUNYANYASA WATOTO

WANAUME ACHENI KUNYANYASA WATOTO

Wakina Baba nchini wametakiwa kuacha tabia za kuwanyanyasa watoto wao wakuwazaa na kuwatelekeza kwa visingizio mbalimbali hali inayopekekea ongezeko la watoto waishio mitaa.

Rai hiyo imetolewa jijini Dar es Salaam na Mkurugenzi Mtendaji wa kituo cha kulelea watoto wenye uhitaji cha Watoto wetu Tanzania, kilichopo Mbezi, Evans Tegeta wakati akipokea msaada wa mahitaji muhimu kutoka Shirika la Nyumba la Taifa (NHC), kuelekea sikukuu ya Mwaka mpya.

“Kina Baba wanawanyanyasa sana watoto wao wa kuwazaa, wakiume kwa wakike wanawachoma moto na kuwapa adhabu za kijeshi, wanawafukuza na kupelekea ongezeko la watoto wanaoishi mitaani, hii nsio changamoto kubwa inayopelekea watoto kuja hapa”

Aidha, akizungumza baada ya kukabidhi msaada huo ukiwemo wa magodoro, vyakula na mavazi Afisa Uhusiano wa Shirika la Nyumba la Taifa, Yamlihery Ndullah amesema NHC itaendelea kuwa sambamba na watoto wenye uhitaji katika kuhakikisha wanafikia ndoto zao.

Previous articleMAGAZETI YA LEO JUMAMOSI DISEMBA 31-2022
Next articlePAPABENEDICT  WA XVI AFARIKI DUNIA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here