Home LOCAL MAJALIWA AHANI MSIBA WA MHE. CLEOPA DAVID MSUYA

MAJALIWA AHANI MSIBA WA MHE. CLEOPA DAVID MSUYA

Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Mei 8, 2025 amehani msiba wa aliyekuwa Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Cleopa David Msuya, Upanga Jijini Dar es Salaam.

Akizungumza na wanafamilia pamoja na waombolezaji wengine, Mheshimiwa Majaliwa, amewasihi kuendelea kumuombea Mhe. Msuya na wawe wavumilivu katika kipindi hiki kigumu.

Marehemu Cleopa Msuya alifariki Mei 07, 2025 katika hospitali ya Mzena Jijini Dar es Salaam, alipokuwa akipatiwa matibabu.