Home LOCAL DKT. NCHIMBI, WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU CCM WASIMAMA KWA DAKIKA MOJA KWA...

DKT. NCHIMBI, WAJUMBE WA HALMASHAURI KUU CCM WASIMAMA KWA DAKIKA MOJA KWA AJILI YA HESHIMA KWA HAYATI MSUYA

Thank you for reading this post, don't forget to subscribe!

Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Balozi Dkt. Emmanuel John Nchimbi, akiwaongoza Wajumbe wa Sekreterieti ya Halmashauri Kuu ya CCM Taifa, kusimama kimya kwa dakika moja, kwa ajili ya heshima ya Hayati Mzee David Cleopa Msuya, Makamu wa Kwanza wa Rais na Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, ambaye pia aliwahi kuwa Mjumbe wa Kamati Kuu na Mbunge wa CCM. Sekreterieti hiyo chini ya uenyekiti wa Balozi Nchimbi, imekutana katika kikao maalum kilichofanyika Ofisi ya Makao Makuu ya CCM, jijini Dodoma, leo Alhamis tarehe 8 Mei 2025.