Home BUSINESS BoT: TAASISI ZA FEDHA ZINAPASWA KUWAKOPESHA WAKULIMA

BoT: TAASISI ZA FEDHA ZINAPASWA KUWAKOPESHA WAKULIMA

Afisa Mkuu Mwandamizi, Kurugenzi ya Usimamizi Sekta ya Fedha, Idara ya huduma ndogo ya Fedha, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Deogratius Mnyamani, akizungumza kwenye mahojiano na waandishi wa Habari katika maonesho ya N

Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imesema itaendelea kutengeneza mazingira rafiki kwa wakulima katika kuhakikisha wanapata mikopo kwa riba nafuu ili waweze kufikia malengo na kupiga hatua katika nyanja mbalimbali za maendeleo.

Akizungumza kwenye mahojiano katika Maonesho ya kimataifa ya kilimo Nanenane yanayofanyika Nzuguni jijini Dodoma, Afisa Mkuu Mwandamizi, Kurugenzi ya Usimamizi Sekta ya Fedha, Idara ya huduma ndogo ya Fedha, Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Bw. Deogratius Mnyamani, amesema kuwa BoT imetenga fedha kwa ajili ya taasisi za fedha ikiwemo mabenki ili waweze kuwakopesha wakuilimo kwa riba nafuu.

Amesema kuwa lengo ni kuhakikisha wakulima wanapata mikopo kwa gharama nafuu ili kuleta tija kwa Taifa katika sekta ya kilimo.

Amesema kuwa ili mkulima apige hatua katika mafanikio anatakiwa kuwa mipango pamoja na kufanya uwekezaji katika sekta ya kilimo jambo ambalo litaleta tija na kufikia malengo husika.

Amesisitiza kuwa taasisi za fedha zinapaswa kutoa mikopo kwa wakulima kwa kuzingatia riba nafuu ili kuhakikisha malengo yanafikiwa.

“Pia kuna fursa mbalimbali kwa wale ambao wanataka kuanzisha biashara za huduma za fedha katika maeneo mbalimbali ikiwemo vijijini kwa kuwakopesha wakulima wadogo”

Previous articleEPZA YAHAMASISHA WAWEKEZAJI WANDANI KUTUMIA FURSA WALIZONAZO
Next articleFCS NA TCRA-CCC WASAINI MAKUBALIANO KUWALINDA WATUMIAJI HUDUMA SEKTA ZA MAWASILIANO
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here