Home LOCAL WAHANDISI WASHAURI NCHINI WATAKIWA KUSIMAMIA KWA UKARIBU UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA

WAHANDISI WASHAURI NCHINI WATAKIWA KUSIMAMIA KWA UKARIBU UJENZI WA MIUNDOMBINU YA BARABARA

Tabora

Naibu Katibu Mkuu anayesimamia miundombinu OR-TAMISEMI Mhandisi Rogatus Mativila amewataka Wahandisi Washauri wanaosimamia miradi mbalimbali ya miundombinu ya barabara nchini kusimamia kwa ukaribu miradi hiyo ili ikamilike kwa wakati.

Mhandisi Mativila ameyasema hayo leo tarehe 10 Juni,2024 wakati akikagua ujenzi wa jengo la ofisi la wahandisi katika manispaa ya Tabora ambalo lipo chini ya mradi wa TACTIC unaosimamiwa na TARURA.

“Mhe. Rais Dkt. samia Suluhu Hassan anahangaika kutafuta fedha ili kuhakikisha wananchi wanapata barabara, wataalam lazima mbadilike na kusimamia kwa ukaribu ujenzi wa miradi hii. Mkandarasi huyu angekuwa anasimamiwa kwa ukaribu angeshakuwa amemaliza hapa”.

Hata hivyo Mhandisi Mativila amewataka wataalam hao kuhakikisha wanasimamia ubora wa ujenzi ili wakandarasi wakamilishe kazi kwa wakati.

Aidha, amemtaka Mhandisi Mshauri UNITEC Civil Consultants ltd kuhakikisha anasimamia kwa karibu ujenzi huo na ifikapo mwezi Agosti mwaka huu jengo hilo liwe limekamilika.

Ujenzi wa jengo la ofisi la wahandisi linalogharimu takriban milioni 800 lilianza ujenzi wake Novemba 2023 na lilitarajiwa kukamilika 15 Juni,2024 na kuagiza ujenzi huo uwe umekamilika ifikapo Agosti 2024 na linajengwa na mkandarasi CICO Contractor.

Previous articleWANNE WAKAMATWA WAKITOROSHA MIFUGO 70 KWA NJIA ZA PANYA ROAD LONGIDO
Next articleBVR KITS 6,000 KUBORESHA DAFTARI LA WAPIGA KURA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here