Home LOCAL SERIKALI YAMUITIKIA MTATURU BUNGENI

SERIKALI YAMUITIKIA MTATURU BUNGENI

MBUNGE wa Singida Mashariki Miraji Mtaturu ameihoji serikali ni lini itapeleka fedha kwa ajili ya ukarabati wa Shule Kongwe zilizopo katika Jimbo lake.

Mtaturu ameuliza swali hilo Juni 28,Bungeni katika kipindi cha maswali na majibu,“ Mh Spika,Shule za Dung’unyi na Kinyamwandyo katika Jimbo la Singida Mashariki ni shule kongwe na zimechakaa,Je ni lini serikali italeta fedha kwa ajili ya kuzikarabati shule hizo,?”.amehoji Mtaturu.

Akijibu swali hilo Naibu Waziri,Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa(TAMISEMI),Zainabu Katimba amesema serikali imekuwa ikifanya ukarabati katika shule zote kongwe nchini na tayari imeanza kuhudumia maeneo mbalimbali.

“Na wewe Mh Mbunge nikuhakikishie kuwa,katika jimbo lako kwa sababu kuna shule hizi chakavu fedha zitaletwa kwa ajili ya kuhakikisha miundombinu inaboreshwa na shule zako zinakarabatiwa,”.amesema.

Previous articleRAIS MWINYI AZINDUA BOBARI YA KUHIFADHI NISHATI SAFI YA OREXY ZANZIBAR
Next articleBENKI YA CRDB YAADHIMISHA SIKU YA WAJASIRIAMALI DUNIANI IKITOA SHILINGI BILIONI 995 MPAKA MEI 2024
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here