Home BUSINESS BRELA YATOA ELIMU MAONESHO YA MUUNGANO JIJINI DAR

BRELA YATOA ELIMU MAONESHO YA MUUNGANO JIJINI DAR

Afisa Usajili wa Wakala wa Usajili wa Kampuni na Leseni (BRELA), Ruth Mbaga (kushoto) akitoa elimu kwa mkazi wa Jiji la Dar es Salaam, Abibu Jitwe (kulia), alipofika kupata elimu, katika Banda la taasisi hiyo kwenye maonesho ya Muungano yanayoendelea Jijini Dar es Salaam.

Na: Hughes Dugilo. DAR

Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA), umeendelea kutoa elimu kwa wananchi mbalimbali wanaotembelea kwenye maonesho ya miaka Sitini (60) ya Muungano wa Tanganyika na Zanizabar, yayofanyika kwenye viwanja vya Mnazi mmoja Jijini Dar es Salaam.

Maonesho hayo yamefunguliwa rasmi Aprili 19, mwaka huu, ambapo yamekutanisha taasisi mbalimbali zikiwemo zile za Muungano.

Akizungumza katika Maonesho hayo, Afisa Usajili wa BRELA Ruth Mbaga, amesema maonesho hayo yanatoa fursa kwa wananchi kupata elimu juu ya kazi wanazofanya sambamba na kupata huduma za papo kwa hapo ikiwemo usajili wa Kampuni na majina ya Biashara.

BRELA, imekuwa na uhusiano mzuri na Wakala wa Usajili wa Mali na Biashara Zanizabar, (BPRA), katika nyanja mbalimbali ikiwemo usajili wa alama za Biashara na Huduma, pamoja na Hataza.

Pia Kwenye Leseni za Viwanda na Biashara, kwa zile Biashara zenye sura ya Kitaifa na Kimataifa.

Maonesho hayo yamezinduliwa  April 19 ambapo yatafungwa rasmi April 25, mwaka huu

Previous articleWAZIRI MKUU AONYA KUHUSU RUSHWA KITEGA UCHUMI CHA STENDI YA KANGE
Next articleSERIKALI IMEFANYA MAKUBWA MIAKA 60 YA MUUNGANO- HOMERA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here