Home LOCAL KITUO CHA JEMOLOJIA (TGC) CHAINGIZWA KATIKA ORODHA YA WANUFAIKA WA BODI YA...

KITUO CHA JEMOLOJIA (TGC) CHAINGIZWA KATIKA ORODHA YA WANUFAIKA WA BODI YA MIKOPO (HESLB)

Jumanne Shimba Kaimu Mratibu wa  Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) jijini Arusha  akizungumza katika kikao kazi na waandishi wa habari ambao wapo kwenye ziara ya kutembelea miradi ya kituo hicho.

Jumanne Shimba Kaimu Mratibu wa  Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) jijini Arusha  akifafanua jambo wakati akizungumza katika kikao kazi na waandishi wa habari ambao wapo kwenye ziara ya kutembelea miradi ya kituo hicho.

Mwaka wa fedha  2023/2024 Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) kimeingizwa katika orodha ya wanufaika wa mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu HESLB ambapo wanafunzi 11 tayari wamenufaika na mikopo hiyo.

Hayo yameelezwa leo Machi 20, 2024 Jumanne Shimba Kaimu Mratibu wa  kituo katika  kituo hicho jijini Arusha  katika kikao kazi na waandishi wa habari ambao wapo kwenye ziara ya kutembelea miradi ya kituo hicho.

Amesema Wanafunzi  349 waliohitimu mafunzo ya fani mbalimbali za uongezaji thamani madini kutoka Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) wamepata fursa za ajira ikiwemo kujiajiri katika maeneo mbalimbali nchini.

“Vijana wengi ambao wamehitimu katika kituo hiki wamepata nafasi ya kuajiriwa na kujiajiri ikiwemo katika kampuni zinazofanya shughuli za uongezaji thamani kutokana na kuwa na ujuzi wa kiwango cha juu.”

Amesema, idadi hiyo ya wahitimu ni tangu kituo hicho ambacho kina usajili rasmi wa Baraza la Taifa la Elimu ya Ufundi na Mafunzo ya Ufundi Stadi (NACTVET) kianze kutoa mafunzo mwaka 2015.

Shimba amesema, kituo hicho kinatoa mafunzo ya muda mfupi katika fani ya ukataji na ung’arishaji wa madini ya vito, fani ya usonara, fani ya uchongaji wa vinyago vya vito.

Pia, utambuzi wa madini ya vito na utengenezaji wa bidhaa za mapambo na urembo ili kuongeza tija katika sekta ya madini na kuwapa fursa za ajira Watanzania.

“Sisi tunachowafundisha ni pale madini yanapotoka mgodini kuanza kuyafanyia uchambuzi mpaka pale ambapo madini yanafikia kuwa bidhaa, baada ya kuyaongezea thamani madini hadi kwenda kumfikia mteja.”

Aidha, Shimba amesema, katika mwaka wa fedha kituo kimeingizwa katika orodha ya wanufaika wa mikopo kutoka Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu.

“Kwa hiyo mwaka huu wanafunzi 11, wameweza kunufaika na mkopo huo, na tunatarajia wanafunzi wengi zaidi kuweza kunufaika.”

Malengo ya TGC ni kudumisha ubora, viwango, uadilifu na taaluma katika utoaji wa huduma zinazohusiana na madini ya vito ili kufikia viwango vinavyotakiwa katika soko la Kimataifa.

Ziara hii ya siku sita katika kituo cha TGC inawajumuhisha waandishi wa habari za mtandaoni kutoka vyombo mbalimbali kwa lengo la kujifunza shughuli zinazofanywa na kituo hicho

Jumanne Shimba Kaimu Mratibu wa  Kituo cha Jemolojia Tanzania (TGC) jijini Arusha akimsikiliza Bw. Samwel Mtuwa Afisa Habari wizara ya Madini.

Picha mbalimbali zikionesha waandishi wa habari wakiagalia shughuli za kituo hicho wakati walipotembelea na kujionea  shughuli mbalimbali.

Previous articleWATANZANIA WANAJIVUNIA MIAKA 3 YA UWEZO MKUBWA; NCHIMBI
Next articleTMX YAPAISHA MAPATO KAGERA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here