Home SPORTS MALI YAICHAPA SOUTH AFRICA 2-0 AFCON

MALI YAICHAPA SOUTH AFRICA 2-0 AFCON

Timu ya Taifa ya Mali imeibuka kidedea kwa kupata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Timu ya Taifa ya Afrika Kusini katika mchezo wa kundi E wa michuano ya AFCON inayopigwa nchini Ivory Coast.

Mabao ya Mali yamepachikwa kambani na Nahodha wa timu hiyo Hamali Traole katika dakika ya 60 ya kipindi cha pili cha mchezo huo, akimalizia mpira wa adhabu uliopigwa nje kidogo ya 18 katika lango la Afrika Kusini.

Iliwachukua dakika 6 tu vijana wa Mali kupata bao la pili lilipachikwa kambani na Lassine Sinayoko katika dakika ya 66 ya mchezo huo.

Mtanange huo uliopigwa katika Dimba la Amadou Curibari ulianza kwa kasi kwa timu zote kucheza kwa nidhamu ya juu, huku Afrika ya Kusini ikicheza kwa kushambulia na kufanikiwa kupata mkwaju wa penati katika ya 19, ambapo Percy Tau alipaisha na kupoteza nafasi hiyo.

Kufuatia mchezo huo, Mali wameshika uongozi wa kundi E ikiwa na alama 3, ikifuatiwa na Namibia alama 3, huku Tunisia na Afrika Kusini wakiwa na alama 0.

Previous articleRAIS SAMIA AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI
Next articleSOMA MAGAZETI YA LEO JUMATANO JANUARI 17-2024
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here