Home SPORTS WAZIRI MKUU AKABIDHI HUNDI YA SHILINGI MILIONI 500 KWA TAIFA STARS

WAZIRI MKUU AKABIDHI HUNDI YA SHILINGI MILIONI 500 KWA TAIFA STARS

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akimkabidhi Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia hundi ya Shilingi milioni 500 ikiwa ni ahadi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu, Taifa Stars baada ya kufuzu michuano ya AFCON ya mwaka 2024. Makabidhiano hayo yalifanyia katika uwanja wa Taifa wa Benjamin Mkapa jijini Dar es salam, Oktoba 4, 2023. Wa pili kushoto ni Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Dar es salaam, Albert Chalamila. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka wa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro (kushoto) kuhusu ukarabati wa Uwanja wa Taifa wakati alipokagua ukarabati huo jijini Dar es salaam, Oktoba 4, 2023. Kushoto kwake Rais wa Shrikikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu).

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka wa Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Damas Ndumbaro (wa tatu kushoto) kuhusu ukarabati wa Uwanja wa Taifa wakati alipokagua ukarabati huo jijini Dar es salaam, Oktoba 4, 2023. Kushoto kwake Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza katika hafla ya kukabidhi hundi ya Shilingi milioni 500 ikiwa ni ahadi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa Timu ya Taifa ya Mpira wa Miguu, Taifa Stars baada ya timu hiyo kufuzu michuano ya AFCON ya mwaka 2024. Hafla hiyo ilifanyika kwenye uwanja wa Taifa jijini Dar es salaam, Oktoba 4, 2023. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Previous articleTANZANIA YASHIRIKI MKUTANO WA SHIRIKA LA MAKAZI ALGERIA
Next articleMABORESHO YALIYOFANYWA KITUO CHA AFYA LUKOMBE YAPUNGUZA RUFAA ZA WAGONJWA MTWARA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here