Home BUSINESS TAMKO LA KAMATI YA SERA YA FEDHA YA BENKU KUU YA TANZANIA 

TAMKO LA KAMATI YA SERA YA FEDHA YA BENKU KUU YA TANZANIA 

Kamati ya Sera ya Fedha (MPC) ya Benki Kuu ilifanya mkutano wake wa 228 tarehe   Fax No. 2234217 

27 Oktoba 2023, kutathmini utekelezaji wa sera ya fedha na mwenendo na mwelekeo  wa uchumi. Kamati ilibaini kuwa utekelezaji wa sera ya fedha ulichangia kuwepo kwa  kiasi cha kutosha cha ukwasi kwenye uchumi kwa mwezi Agosti, Septemba na Oktoba 2023. Utekelezaji wa sera ya fedha, pamoja na sera thabiti za kibajeti, na kimfumo, zimesaidia kukabiliana na shinikizo la mfumuko wa bei, kuchangia ukuaji wa shughuli  za kiuchumi na uhimilivu wa sekta ya fedha nchini licha ya mtikisiko wa kiuchumi  duniani. Utekelezaji wa sera ya fedha pia umesaidia kupunguza shinikizo linalotokana  na ongezeko la mahitaji ya fedha za kigeni nchini.  

Kamati pia, ilitathmini mwenendo wa uchumi wa dunia kwa mwaka 2023 na kubaini  kuwa, uchumi wa dunia bado haujaimarika licha ya ukuaji wa juu ya matarajio  uliofikiwa katika kipindi cha nusu ya kwanza ya mwaka. Mwenendo huu unatokana na kubanwa kwa sera ya fedha katika nchi nyingi duniani, migogoro ya kisiasa na  ongezeko la bei za mafuta. Mfumuko wa bei umepungua kutoka viwango vilivyofikiwa  mwaka 2022, licha ya kubakia juu ya malengo kwa nchi nyingi. Ili kuhakikisha  mfumuko wa bei unabakia ndani ya malengo, nchi nyingi zimeendelea kutekeleza sera  ya fedha yenye lengo la kupunguza ukwasi.  

Katika kutathmini mwenendo wa uchumi hapa nchini, Kamati ilibaini kuwa:  

  1. Pato la Taifa kwa Tanzania Bara lilikua kwa kiwango cha kuridhisha cha asilimia  5.4 na asilimia 5.2 katika robo ya kwanza na ya pili, mtawalia na kuna matarajio  ya kufikia makadirio ya ukuaji wa asilimia 5.3 kwa mwaka 2023. Kwa upande  wa Zanzibar, uchumi ulikua kwa asilimia 6.2 katika robo ya kwanza ya 2023,  na kuna uwezekano mkubwa wa kufikiwa kwa lengo la ukuaji wa asilimia 7.1  kwa mwaka 2023. 
  2. Mfumuko wa bei kwa Tanzania Bara umepungua na kufikia asilimia 3.3 mwezi  Septemba 2023, kutoka asilimia 3.6 mwezi Juni 2023, ukichangiwa na  kupungua kwa bei za vyakula. Kwa upande wa Zanzibar, mfumuko wa bei  ulikuwa asilimia 7.5 ukilinganisha na asilimia 6.5 mwezi June 2023,  

  1 ukichangiwa na ongezeko la bei za vyakula. Mfumuko wa bei   unatarajiwa  kuendelea kuwa ndani ya lengo la muda wa kati la   asilimia 5, licha ya ongezeko  la bei za mafuta hivi karibuni. 

iii. Ukuaji wa ujazi wa fedha (M3) ulikuwa wastani wa asilimia 17.7 kwa robo ya  kwanza ya mwaka 2023/24 juu ya makadirio ya ukuaji wa asilimia 10.1 kwa  mwaka unaoishia Desemba 2023. Mwenendo huu ulitokana na ukuaji wa  mikopo kwa sekta binafsi ambao ulifikia takriban asilimia 22 kwa kipindi cha  mwezi Julai na Agosti na asilimia 19.5 mwezi Septemba 2023, ukilinganisha na 

makadirio ya ukuaji wa asilimia 16.4 kwa mwezi Desemba 2023. Ukuaji wa  mikopo kwa sekta binafsi ulitokana na ongezeko la mahitaji ya mikopo mipya  kufuatia kuimarika kwa mazingira ya biashara nchini, ukichagizwa na  utekelezaji thabiti wa sera ya fedha. Aidha, shughuli za kilimo zimeendelea  kunufaika kwa kiwango kikubwa na ongezeko la kasi ya ukuaji wa mikopo kwa  sekta binafsi.  

  1. Ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa Tanzania Bara ulikuwa wa kuridhisha  ambapo makusanyo yalifikia asilimia 96.2 ya lengo katika robo ya kwanza ya  mwaka 2023/24. Kwa upande wa Zanzibar, ukusanyaji wa mapato ulivuka  lengo kwa asilimia 1.7. Matumizi ya Serikali yameendelea kufanyika kulingana  na mapato. 
  2. Nakisi ya urari wa biashara, huduma na uhamisho mali nje ya nchi imeendelea  kuwa kubwa kutokana na kupanda kwa bei za bidhaa katika soko la dunia. Hata  hivyo nakisi hii ilipungua kufikia dola milioni 3,652.6 kwa mwaka unaoishia  Septemba 2023, kutoka dola milioni 4,728.1 kwa mwaka ulioishia Septemba  2022, kutokana na ongezeko la mapato yanayotokana na shughuli za utalii. 

Nakisi hii inatarajiwa kupungua zaidi kutokana na kuendelea kuongezeka kwa  mapato yatokanayo na shughuli za utalii, mauzo ya dhahabu na mazao ya  biashara nje ya nchi. Kwa upande wa Zanzibar nakisi ya urari wa biashara,  huduma na uhamisho mali nje ya nchi ilifikia dola za Marekani milioni 417.1  ukilinganisha na dola za marekani milioni 344.4, kutokana na ongezeko la  gharama za uagizaji wa bidhaa na huduma kutoka nje ya nchi.  

  1. Akiba ya fedha za kigeni imeendelea kubaki katika viwango vya kuridhisha vya  takribani dola za Marekani bilioni 5 katika kipindi cha mwezi Julai mpaka  Oktoba 2023, kiwango kinachotosha kugharamia uagizaji wa bidhaa na 

   2 huduma nje ya nchi, juu ya viwango vya nchi na jumuiya ya       Afrika Mashariki  vya miezi 4 na 4.5 mtawalia. 

vii. Sekta ya benki iliendelea kuwa na mtaji, ukwasi wa kutosha na inayotengeneza  faida. Ubora wa rasilimali umeendelea kuimarika, kufuatia kupungua kwa  viwango vya mikopo chechefu kufikia asilimia 5.2 mwezi Septemba 2023,  kutoka asilimia 7.3 mwezi Septemba 2022. Kupungua kwa viwango vya mikopo  chechefu kunategemewa kuongeza chachu ya ukuaji wa mikopo kwa sekta  binafsi.  

Kamati pia, ilibaini uhaba wa fedha za kigeni ulioonekana hivi karibuni nchini umeendelea kupungua kufuatia ongezeko la mapato yatokanayo na shughuli za utalii,  mauzo ya dhahabu na mazao ya biashara nje ya nchi. Uuzaji wa fedha za kigeni  uliofanywa na Benki Kuu kwa lengo la kukabiliana na ongezeko la mikopo inayotokana  na uagizaji wa bidhaa nje ya nchi pia umepunguza changamoto hii. Hali ya upatikanaji  wa fedha za kigeni inatarajiwa kuendelea kuimarika kutokana na matarajio ya mapato  yanayotokana na shughuli za utalii, uuzaji wa madini na mazao ya biashara, pamoja  na hatua zinazochukuliwa na Benki Kuu na Serikali katika kukabiliana na changamoto  ya upungufu wa fedha za kigeni.  

Kwa kuzingatia mwenendo wa uchumi wa dunia na wa hapa nchini, Kamati ya Sera  ya Fedha iliamua kuendelea na utekelezaji wa sera ya fedha inayolenga kupunguza  kasi ya ongezeko la ukwasi katika uchumi. Sera ya fedha itaendelea kutekelezwa  sambamba na sera za kibajeti na kimuundo ili kufikia malengo ya kiuchumi. Aidha, utekelezaji wa Sera ya Fedha unalenga kuhakikisha malengo yaliyoainishwa kwenye  programu ya Extended Credit Facility (ECF) kwa robo inayoishia Desemba 2023  yanafikiwa. 

GAVANA 

BENKI KUU YA TANZANIA

Previous articleMSD KANDA YA IRINGA YAKABIDHI VIFAA TIBA KITUO CHA AFYA KIFANYA
Next articleMAJALIWA ATOA MAAGIZO KWA BODI YA MIKOPO ELIMU YA JUU (HESBL)
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here