Home BUSINESS HAKIKISHENI MWANACHAMA PSSSF ASIONDOKE OFISINI KWETU HAJARIDHIKA: CPA. KASHIMBA

HAKIKISHENI MWANACHAMA PSSSF ASIONDOKE OFISINI KWETU HAJARIDHIKA: CPA. KASHIMBA

NA
K-VIS BLOG, DAR ES SALAA.

MKURUGENZI
Mkuu wa Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma, (PSSSF), CPA. Hosea
Kashimba, amewataka watumishi wa Mfuko huo kuhakikisha kwamba mwanachama
anapofika ofisini kuhudumiwa asiondoke hajaridhika.

Ameyasema
hayo jijini Dar es Salaam, Oktoba 6, 2023 kwenye kilele cha maadhimisho wa Wiki
ya Huduma kwa Wateja, alipokuwa akizungumza na watumishi wa PSSSF ofisi ya Kanda
ya Kinondoni.

“Ombi
langu kwenu, ule utaratibu mwanachama akiwa na tatizo anaambiwa andika barua,
hatuuhitaji hapa, hizo ni taratibu za kizamani, tutatue matatizo ya wanachama
wetu haraka.” Alisema.

Alisema
ukigundua kuna tatizo, litatue, ukimwambia mwanachama aandike barua
unamshawishi alalamike, tuhakikishe tatizo lisiwe upande wetu, huo ndio mtizamo
wetu na hata kama litakuwa upande wa pili tujitahidi kulifuatilia sisi wenyewe
na kulitatua, alisisitiza CPA. Kashimba.

Alisema
watumishi wa PSSSF, popote walipo nchini, wahakikishe hakuna tatizo la mwanachama
linalala halijatatuliwa.

Kuhusu
uboreshaji wa utoaji huduma, CPA. Kashimba amewahakikishia wanachama azma ya
Mfuko ni kuhakikisha wanatumia mifumo ya TEHAMA kupunguza kuonana na wanachama.

“Niwaambie
wateja wetu kuanzia Juni mwakani, tumedhamiria kupunguza kuonana na wanachama, tunataka
uwasilishaji madai unafanyika online, kuyachakata online, mwanachama akutane na
fedha yake benki na hilo tayari tumelianza,” alisema na kuongeza…nia
hapa ni kumuondolea mwanachama gharama za kufuata huduma kwenye ofisiz etu,
kuokoa muda, lakini pia kupunguza
matumizi ya karatasi,
na kwa vile karatasi ni miti, tutakuwa tumeokoa mazingira na hivyo kuisaidia
Serikali katika kutunza mazingira yetu.” Alifafanua.

Aidha,
CPA.  Kashimba, amepongeza ushirikiano
baina ya taasi yake na zile za Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) na
Shirika la Taifa la Hifadhi ya Jamii (NSSF), wakati wa Maadhimisho ya Wiki ya
Huduma kwa Wateja.

Wiki
ya Huduma kwa wateja ni tukio la kimataifa ambalo linaangazia umuhimu wa huduma
kwa wateja na watu wanaotoa huduma kwa lengo la kuimarisha ushirikiano kwa
watoa huduma na wateja na kauli mbiu ya mwaka huu ni TEAM SERVICE “Ushirikiano
kwa Huduma Bora.”

“Team
service ni ushirikiano wa kutoa huduma, tunapokuwa kama timu inasaidia kujibu
hoja za wanachama wetu, vizuri na kwa haraka, ndio maana tumekuwa na watu wa
NIDA , ambao wametusaidia sana kutatua changamoto za vitambulisho vya taifa kwa
wanachama wetu takriban 36 hivi.” Alisema.

Alisema,
“Wanachama wetu hawa wamehudumiwa wakiwa
hapa na hawakuhitaji kwenda ofisi za NIDA.” Alisema

Hata
wenzetu wa NSSF, ushirikiano tulio nao ni kama timu moja, jambo likiwa kwetu,
lakini linahitaji uingiliaji wa NSSF, tunaweza kuliona, kwa hiyo ujumbe wa
mwaka huu unatafsiri ushirikiano huu wa kitaasisi.” Alisema CPA. Kashimba.

Alisema
ushirikiano kama huu umekuwepo hata kwenye maonesho mbalimbali kama vile
Sabasaba, Nane nane na kwingineko, ambapo Mifuko ya PSSSF na NSSF wamekuwa
wakikaa pamoja ili kurahisisha utoaji wa huduma kwa wateja wao.

Mkurugenzi Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba, akizungumza kwenye hafla hiyo.

Mkurugenzi
Mkuu wa PSSSF, CPA. Hosea Kashimba (kulia), akimkabidhi cheti cha shukrani
(Appreciation), Afisa wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA), Wilaya ya
Knondoni, Bi. Zuwena Abdallah, kwa ushirikiano walioutoa wakati wa wiki ya
huduma kwa wateja, 2023. Kushoto ni  Mkurigenzi
wa Uendeshaji wa Mfuko wa PSSS, Bw. Mbaruku Magawa, na Meneja wa Kanda
wa PSSSF Kinondoni, Bi. Ritha Ngalo.

CPA. Kashimba (wakwanza kushoto) kwa karibu akiwa na Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbaruku Magawa (wapili kushoto), akichukua maoni ya mwanachama

Mkurugenzi wa Uendeshaji PSSSF, Bw. Mbaruku Magawa, akizungumza kwenye hafla hiyo.

Meneja wa Kanda wa PSSSF Kinondoni, Bi. Ritha Ngalo (kushoto), akimuhudumia mteja (mwanachama) wa PSSSF.

CPA. Kashimba akipitishwa kwenye eneo la NSSF ambao nao waliungana na PSSSF kuhudumia wanachama.

Previous articleYASEMAVYO MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI OCTOBA 7-2023
Next articleDIWANI ASHA JOHARI AWATAKA WAZAZI ILALA KUWALEA WATOTO KIMAADILI 
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here