Home LOCAL WAZIRI MKUU MSTAAFU MIZENGO PINDA AAHIDI KUSHIRIKI UJENZI WA BWENI LA WANAFUNZI...

WAZIRI MKUU MSTAAFU MIZENGO PINDA AAHIDI KUSHIRIKI UJENZI WA BWENI LA WANAFUNZI WA KIKE CHUO KIKUU MZUMBE

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Rais Chakula na Kilimo Mh. Peter Mizengo Pinda akisaini kitabu cha wageni wakati alipotembelea banda la Chuo Kikuu cha Mzumbe Leo Agosti 5,2023 kwenye Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Nanenane yanayofanyika kwenye viwanja vya John Mwakangale Jijini Mbeya kulia ni Bwana Aloyce Gervas, Mwakilishi wa Kurugenzi ya Ukimataifishaji na Baraza la Wahitimu Chuo Kikuu Mzumba na kushoto ni Dk. Nicholaus Tutuba Kaimu Meneja wa Kitengo cha Ubunifu, Ujasiriamali na Ushirikiano wa Viwanda wa Chuo Kikuu Mzumbe. 

Mhe. Misengo Pinda ametembelea Banda la Chuo Kikuu hicho kwa lengo la kujionea shughuli mbalimbali za kitaaluma na ubunifu.

Aidha amejulishwa kuhusu kampeni ya ujenzi wa hosteli ya wanafunzi wa kike Ndaki ya Mbeya na ameahidi kushiriki.

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Rais Chakula na Kilimo Mh. Peter Mizengo Pinda akizungumza jambo na Dk. Nicholaus Tutuba Kaimu Meneja wa Kitengo cha Ubunifu, Ujasiriamali na Ushirikiano wa Viwanda wa Chuo Kikuu Mzumbe wakati alipotembelea Katika banda la Chuo Kikuu Mzumbe katika Maonesho ya Kimataifa ya Kilimo Jijini Mbeya. 

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Rais Chakula na Kilimo Mh. Peter Mizengo Pinda akiangalia Bidhaa mbalimbali katika banda hilo. 

Waziri Mkuu Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mwenyekiti wa Baraza la Ushauri la Rais Chakula na Kilimo Mh. Peter Mizengo Pinda akipata maelezo Kutoka kwa Bi. Gloria  Mushi, Afisa Masoko Chuo Kikuu Mzumbe.

Previous articleKUNDI JIPYA LAIBUKA NGORONGORO, WATAKA WALIPWE FIDIA WAHAMIE WANAKOTAKA WAO
Next articleNAIBU KATIBU MKUU KILIMO DKT. HUSSEN ATEMBELEA BANDA LA OFISI YA WAZIRI MKUU NANE NANE MBEYA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here