Home LOCAL WANAFUNZI WOTE KUPATA MIKOPO YA ELIMU YA JUU

WANAFUNZI WOTE KUPATA MIKOPO YA ELIMU YA JUU

Na: Immaculate Makilika – MAELEZO

Serikali imeendelea kuongeza bajeti ya Mikopo kwa Wanafunzi wa Elimu ya Juu mwaka hadi mwaka ili kuongeza wigo wa wanufaika.

Kauli hiyo imetolewa bungeni Dodoma leo na Naibu Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Mhe. Omary Kipanga wakati akijibu swali la Mbunge wa Viti Maalum, Mheshimiwa Dkt. Thea Medard Ntara aliyeuliza kuhusu mpango wa Serikali wa kuhakikisha wanafunzi wote wanaomaliza kidato cha sita wanapata mikopo ya Elimu ya Juu.

“Bajeti ya Mikopo iliongezeka kutoka Shilingi bilioni 570 mwaka 2021/2022 hadi Shilingi bilioni 654 mwaka 2022/2023. Pia, Mwaka 2022/2023 Shilingi bilioni 3 zilitengwa kwa ajili ya Samia Scholarship iliyonufaisha wanafunzi 593 waliohitimu kidato cha sita wenye ufaulu wa juu kwenye masomo ya Sayansi, Teknolojia, Uhandisi na Hesabu (STEM)”. Alisema Naibu Waziri Kipanga.

Alifafanua kuwa katika kuendelea kupanua fursa za mikopo kwa wahitimu wa kidato cha sita, Serikali imeingia mkataba wa mahusiano na Benki ya NMB ili kutoa mikopo yenye riba nafuu  ya asilimia 9 kwa wazazi au walezi kwa ajili ya kugharamia elimu ya watoto wao katika ngazi ya Elimu ya Juu na Kati.

 “Aidha, Serikali itaendelea kutafuta fursa za Mikopo ya Elimu ya Juu kutoka kwa Wadau mbalimbali ili kuhakikisha kila mhitimu wa kidato cha sita mwenye sifa anapata mkopo kwa ajili ya kugharamia Elimu ya Juu”. Alimaliza Naibu Waziri Kipanga.

Previous articleKATIBU MKUU CHONGOLO AMTEMBELEA BALOZI WA KATA YA BWAWANI KONDOA
Next articleHOJA YA BANDARI YATIKISA MDAHALO WA KITAIFA JIJNI DAR
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here