Home BUSINESS GGML YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUTOA ELIMU KUHUSU AINA ZA...

GGML YAADHIMISHA SIKU YA MAZINGIRA DUNIANI KWA KUTOA ELIMU KUHUSU AINA ZA TAKA, UGAWAJI VIFAA

Ofisa Uhusiano wa GGML, Dafroza Manyanda (kushoto) akikabidhi vifaa vya usafi kwa Mwenyekiti wa Mtaa wa Uwanja uliopo katika Halmashauri ya Geita, Enos Cherehani

Ofisa Mawasiliano Mwandamizi kutoka GGML, Laurian Pima akizungumza na wakazi wa mtaa wa Uwanja katika Halmashauri ya Geita na kuwaelimisha kuhusu umuhimu wa kutenganisha taka za plastiki ili kulinda mazingira ikiwa ni muendelezo wa jitihada za kampuni hiyo katika kuhifadhi mazingira.

Na: Mwandishi wetu, GEITA

KAMPUNI ya Geita Gold Mining Limited (GGML), moja ya migodi maarufu ya AngloGold Ashanti nchini Tanzania, imeadhimisha Siku ya Mazingira Duniani kwa kutoa elimu kuhusu aina mbalimbali za taka za plastiki na ugawaji wa vifaa vya kuhifadhi taka kwa lengo la kuwawezesha wananchi kutenganisha ipasavyo taka za plastiki.

Siku ya Mazingira Duniani ambayo huadhimishwa kila mwaka Juni 5 ni tukio muhimu la kimataifa lililoandaliwa na Mpango wa Mazingira wa Umoja wa Mataifa, na mwaka huu kauli mbiu ni “Tokomeza uchafuzi wa mazingira unaotokana na taka za plastiki”.

Kauli mbiu hiyo inalenga kusisitiza kwamba taka za plastiki ni tatizo la kimataifa ambalo linatishia mazingira, wanyamapori na afya ya binadamu.

Akizungumza katika tukio hilo lililofanyika katika mji wa Geita kwa kuwashirikisha wafanyakazi wa GGML na mamlaka za mitaa, Meneja Mazingira wa Mgodi huo Yusuph Mhando amesema GGML inafahamu uchimbaji madini una athari ya moja kwa moja kwa mazingira kwani rasilimali za ardhi na maji zinahitaji kuendelezwa.

Amesema kampuni hiyo imejidhatiti katika utunzaji wa mazingira na imechukua hatua mbalimbali ili kupunguza mwelekeo wake wa mazingira na kuongeza mchango wake chanya kwa jamii zinazozunguka Geita.

“Moja ya hatua hizo ni usimamizi wa taka za plastiki kutoka vyanzo mbalimbali kama vile vifungashio, vifaa vya kujikinga, chupa za maji na vyombo vya chakula. Kampuni pia inatoa mafunzo kwa wafanyakazi na wakandarasi wote kutenganisha na kutupa aina tofauti za taka kwa kutumia mapipa yenye alama za rangi na lebo. Wafanyakazi wote na wakandarasi hupokea mafunzo ya mazingira ili kuhakikisha uzingatiaji wa sera na taratibu za usimamizi wa taka.

Amesema GGML inafanya kazi kwa pamoja ili kuongeza uelewa kuhusu umuhimu wa kupunguza, kutumia tena na kuchakata plastiki. “Tunajivunia kuadhimisha Siku ya Mazingira Duniani na kushirikisha jamii zinazozunguka mgodi katika kuendeleza desturi nyetu ya kulinda na kuhifadhi mazingira yetu.

“Tunaamini kwa kuwaelimisha na kuwawezesha wananchi kutenganisha ipasavyo taka za plastiki tunaweza kuleta mabadiliko chanya katika vita dhidi ya uchafuzi wa plastiki.Pia tunahimiza kila mtu kuzingatia kanuni ya 3Rs: Punguza, Tumia Tena na Usafishaji plastiki kila inapowezekana,” amesema.

GGML inachukua jukumu lake la kupunguza athari zake za mazingira kwa umakini na imejitolea kuwajibika kwa usimamizi wa mazingira.

Ameongeza mgodi huo umekuwa ukifanya kazi nchini Tanzania kwa zaidi ya miaka 20 na ni miongoni mwa walipakodi wakubwa na wanaokidhi viwango vinavyozingatia sheria nchini. GGML inaajiri zaidi ya watu 5,000 moja kwa moja na kupitia wakandarasi na takriban asilimia 98 kati yao ni raia wa Tanzania.

Previous articleNENKI YA NBC YAZINDUA KOMBE JIPYA LA LIGI KUU SOKA TANZANIA BARA 
Next articleNHC KUSHIRIKI KUBORESHA MIUNDOMBINU YA MICHEZO NCHINI
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here