Home LOCAL TGNP NA DIT KUJA NA SULUHISHO LA MASUALA YA JINSIA KWA NJIA...

TGNP NA DIT KUJA NA SULUHISHO LA MASUALA YA JINSIA KWA NJIA YA KIDIJITALI

.
Mkurugenzi wa Mtandao wa Jinsia Tanzania Lilian Liundi akizungumza wakati wa kufungua semina ya Jukwaa la Wasichana kwenye Vyuo vikuu (Youth Feminist Forum) iliyokuwa na lengo la kujadili changamoto wanazozipata vyuoni pamoja na kuzitafutia utatuzi kupitia Teknolojia iliyofanyika katika ofisi za TGNP Mabibo jijini Dar es Salaam.
Mhadhiri Mwandamizi kutoka Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam(DIT), Dkt. Asinta Manyele akizungumza wakati wa semina ya Jukwaa la Wasichana kwenye Vyuo vikuu (Youth Feminist Forum) ili kujadili namna wanaweza kutatua changamoto wanazozipata vyuoni pamoja na kuzitafutia utatuzi kupitia Teknolojia.
Mkurugenzi wa Taasisi ya Binti Makini na Mwezeshaji wa Semina hiyo Janeth John akiwasilisha mada zinazohusu Uongozi na Utawala kwa mtoto wa kike wakati wa semina ya Jukwaa la Wasichana kwenye Vyuo vikuu (Youth Feminist Forum) ili kujadili namna wanaweza kutatua changamoto wanazozipata vyuoni pamoja na kuzitafutia utatuzi kupitia Teknolojia.
Baadhi ya wanachuo kutoka vyuo mbalimbali wakifuatilia mada wakati wa semina ya Jukwaa la Wasichana kwenye Vyuo vikuu (Youth Feminist Forum) ili kujadili namna wanaweza kutatua changamoto wanazozipata vyuoni pamoja na kuzitafutia utatuzi kupitia Teknolojia.
Afisa Habari na Mawasiliano wa Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP), Monica John akitoa mrejesho wa wakati wa semina ya Jukwaa la Wasichana kwenye Vyuo vikuu (Youth Feminist Forum) ili kujadili namna wanaweza kutatua changamoto wanazozipata vyuoni pamoja na kuzitafutia utatuzi kupitia Teknolojia.
Picha za Pamoja.
Kutokana na makubaliano waloingia kati ya Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) na Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam(DIT) ya kuangalia fursa zilizopo kupitia TEHAMA na ni kwa jinsi gani zinaweza kutatua matatizo ya kijinsia ambayo yanaendelea hapa nchini kwa kukutanisha Jukwaa la Wasichana kwenye Vyuo vikuu (Youth Feminist Forum) ili kuzungumza changamoto wanazozipatia huko vyuoni.
Akizungumza wakati wa kufungua mafunzo hayo Mkurugenzi Mtendaji wa Mtandao wa Jinsia Tanzania Lilian Liundi amesema tuko hapa kuangalia changamoto na kwa namna gani wavhuo wa Taasisi ya DIT wanaweza kuleta suluhisho za hizo changamoto kupitia Teknolojia ili kurahisisha maisha kwenye jamii.
Amesema ikiwa kwa mfano kutatengenezwa mfumo wa kurahisisha kutoa taarifa za ukatili wa kijinsia matukio ya ukatili yatapungua kwasababu hatua za haraka zitachukuliwa na kupatiwa ufumbuzi.
“TGNP tunakuwa na watoto wa Shule za msingi ili kueleza vitu wanavyofanya nyumbani na wazazi wao hivyo kuwepo kwa suala la Teknolojia kwa watoto hao hasa katika kuripoti matukio mbalimbali ambapo mtoto anaweza kwenda kusema na huo mfumo kupeleka taarifa kwenye Mamlaka husika hivyo itasaidia kupunguza masuala ya ukatili wa kijinisia kwenye jamii inayowazunguka kwani watoto wengi ni waoga kuongea na wazazi wake”. Alisema Liundi
Naye Mhadhiri Mwandamizi kutoka Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam(DIT), Dkt. Asinta Manyele amesema leo tunaangalia ni kwa namna gani tunaweza kuitumia Teknolojia ili kutatua matatizo yetu yanayotuzunguka.
Pia ameipongeza TGNP kwa kuwa mwanga wa jamii kwani wanaangaza changamoto za jamii hasa ya kijinsia kwa kuyaweka wazi na kuyachukulia hatua hasa kuyapeleka kwenye mamlaka husika ambapo malengo makubwa ya Taasisi ya Teknolojia ya Dar es Salaam (DIT) ni kujaribu kutatua matatizo ya jamii kupitia teknolojia.
Previous articleDC MPOGOLO AONGOZA KAMPENI YA USAFI ILALA
Next articleFREDERICO WA SINGIDA BIG STARS AONGEZEWA MUDA WA UANGALIZI
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here