Home BUSINESS WANAFUNZI ST.MARY’S WAONESHA VIPAJI MASUAA YA KODI

WANAFUNZI ST.MARY’S WAONESHA VIPAJI MASUAA YA KODI

Mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya Sekondari St Mary’s Mbezi Beach, Sia John akimkabidhi kombe Mwenyekiti wa Bodi ya shule za St Mary’s, Dallas Mhoja, kombe walilopewa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) kwa kuibuka nafasi ya pili kwenye mashindano ya kujibu maswali kuhusu kodi yaliyofanyika hivi karibuni mkoa wa Pwani na kushirikisha shule 59.

Mwanafunzi wa kidato cha nne shule ya sekondari St Maty’s  Mbezi Beach, Sia John akimkabidhi zawadi ys saa, Mwenyekiti wa bodi ya shule hizo Dallas Mhoja sa waliyopewa na TRA kwa kuibuka namba mbili kati ya shule 59 kwenye mashindano ya kujibu maswali kuhusu masuala ya kodi.

Wajumbe wa bodi na walimu wa shule ya St Mary’s High School wakiwa kwenye picha na zawadi walizopewa na TRA kwa shule hiyo kuwa ya pili kati ya shule 59 kwenye shindano la Quiz kuhusu masuala mbalimbali ya kodi iliyofanyika hivi karibuni kwenye chuo cha kodi Mikocheni.

Kamishna Mkuu wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), akimpa zawadi ya ngazo mwanafunzi wa kidato cha nne wa shule ya St Mary’s High School, Sia John baada ya wanafunzi wa shule hiyo kushika  nafasi ya pili kati ya shule 59 katika mashindano ya kujibu maswali kuhusu kodi yaliyofanyika hivi karibuni.

·      Ni katika Quiz iliyoandaliwa na TRA

·       Wajibu maswali ya kodi kwa ufasaha

·      Waibuka nafasi ya pili kati ya shule 59

Na: Mwandishi Wetu.

WANAFUNZI wa shule ya St Mary’s Mbezi Beach jijini Dar es Salaam, wameibuka kidedea kwenye shindano la kujibu maswali mbalimbali yanayohusu kodi.

Shule hiyo iliibuka nafasi ya pili ikitanguliwa na shule ya sekondari ya Kibaha mkoani Pwani katika shindano hilo lililofanyika kwenye Chuo cha Kodi Mikocheni.

Shindano hilo lililodumu kwa siku tatu liliendeshwa hivi karibuni na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) na kushirikisha shule 59 za sekondari binafsi na za umma.

Akizungumzia shindano hilo jana, Mwenyekiti wa bodi ya shule hizo, Dallas Mhoja alisema kufuatia ushindi huo wanafunzi wa shule hiyo walizawadiwa kompyuta, mashine ya kudurufu, kombe na medali mbalimbali.

“Huwa tunashiriki mashindano mbalimbali yanayoandaliwa na TRA kwa hiyo mwaka huu tumeshiriki zilikuwa shule 59 na katika hizo shule tulibuka washindi wa pili nyuma ya Kibaha iliyokuwa ya kwanza,” alisema

Aidha, alisema tukio hilo limefanywa na taasisi kubwa ya serikali kwa kushirikisha shule binafsi na za serikali hivyo ushindi wa shule hiyo ni jambo la kujivunia kwa uongozi mzima wa shule.

Alisema wanafunzi wa shule hiyo walionyesha umahiri wa hali ya juu katika kujibu maswali mbalimbali yanayohusiana na kodi hali iliyowafanya kuibuka wa pili.

“Kushindana na shule 59 za Mkoa wa Dar es Salaam, zikiwemo za binafsi na za serikali na kuibuka kwenye nafasi ya pili tunaona siyo jambo dogo kwetu. Tunajivunia mafanikio haya na mashindano yajayo tutashika namba moja,” alisema

Alitaja siri ya mafanikio hayo kuwa ni maandalizi mazuri ya wanafunzi na walimu wenye kuipenda kazi yao ambao wamekuwa wakifanya kazi usiku na mchana.

“Shindano hili limeleta msisimo mkubwa sana kwa wanafunzi wetu na walimu walioshiriki kwasababu mbali na zawadi kama kompyuta walizawadiwa fedha taslim kwa hiyo mashindano haya ni muhimu sana,” alisema

Mwisho.

Previous articleMLIPUKO WA UINJILISTI WAZINDULIWA DODOMA
Next articleUSHUSHWAJI WA MELI YA MV MWANZA MAJINI UTASAIDIA KUKUZA SEKTA YA UTALII
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here