Home LOCAL BIMA YA AFYA KWA WOTE ITAZINGATIA MASLAHI YA WANANCHI WOTE – DKT.MPANGO

BIMA YA AFYA KWA WOTE ITAZINGATIA MASLAHI YA WANANCHI WOTE – DKT.MPANGO

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango akizungumza na wananchi wa eneo la Kagongwa Wilaya ya Kahama mkoani Shinyanga wakati akiwa ziarani katika mkoa huo leo tarehe 18 Januari.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt, Philip Mpango leo tarehe 18 Januari 2023 akimsalimia na kumpa pole Bi. Prisca Joseph Nyanda mkazi wa Kagongwa wilayani Kahama Mwanamke mwenye ulemavu aliyetelekezwa na Mume wake akiwa na watoto wawili ambao hutembea nao katika baiskeli yake mtaani kutafuta riziki na mahitaji ya watoto hao.

(PICHA: NA OFISI YA MAKAMU WA RAIS)

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. Philip Mpango amesema uamuzi wa Serikali utakaofikiwa baada ya mashauriano ya kina yanayoendelea juu ya kuanzishwa kwa Mfuko wa Bima ya Afya kwa wote utazingatia maslahi ya wananchi wote na hasa wenye kipato kidogo kwa lengo la kumwezesha kila mwananchi kupata huduma bora
za afya na kwa gharama nafuu.

Makamu wa Rais amesema hayo wakati akizungumza na wananchi wa eneo la Kagongwa wilayani Kahama akiwa ziarani mkoani Shinyanga tarehe 18 Januari 2023. Aidha amesema Serikali inaendelea kupokea maoni na ushauri wa watu mbalimbali kuhusu kuanzishwa kwa mfuko huo.

Pia Makamu wa Rais ameutaka uongozi wa mkoa wa Shinyanga kujipanga vizuri zaidi na kusimamia ukusanyaji wa mapato ya Serikali kwa mujibu wa sheria na taratibu zilizowekwa.

Amesema hajaridhishwa na taarifa ya Mkoa kuhusu ukusanyaji wa mapato ya ndani ya halmashauri za Shinyanga.

Aidha Dkt. Mpango Napenda amewasihi wakaguzi wote wa Mkoa pamoja na Baraza la Taifa la Usimamizi wa Mazingira (NEMC) kukagua mabwawa yote ya taka suku mara kwa mara na kufanyia kazi mapema dalili za mabwawa hayo kupasuka ili kuepusha madhara yanayoweza kujitokeza kama ilivyotokea katika eneo la mwadui mkoani humo.

Vilevile amemtaka Mthamini Mkuu wa Serikali kukamilisha uhakiki na uthamini wa mali na mashamba ya wananchi wa mwadui walioathirika na bwawa la taka sumu kupasuka na kuwalipa haki zao haraka iwezekanavyo.

Akiwa katika eneo la Kagongwa,Makamu wa Rais ameagiza kutafutwa na kuchukuliwa hatua mwanaume mmoja aliyejulikana kwa jina la Athuman Yusuph kwa kumtelekeza mwanamke anayefahamika kwa jina la Prisca Nyanda ambaye ni mlemavu akiwa na watoto wawili na hivyo kulazimika kutembea na watoto hao katika baiskeli yake wakati wote akitafuta riziki na mahitaji ya watoto hao.

Makamu wa Rais ametoa shilingi milioni tano wakati akiwaongoza wananchi na viongozi wa eneo hilo katika kumchangia mama huyo fedha zitakazomwezesha kujikimu na kufanya biashara. Zaidi ya shilingi milioni sita na laki nane zimepatikana katika harambee hiyo pamoja na vyakula mbalimbali ikiwemo unga na mchele.

Previous articleTANZANIA NA CHINA ZASAINI MUHTASARI WA TAARIFA YA UPEMBUZI YAKINIFU YA UJENZI NA UPANUZI WA JKCI
Next articleMAKAMU WA RAIS AWEKA JIWE LA MSINGI HOSPITALI YA RUFAA SHINYANGA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here