Home BUSINESS ACCSESS MICROFINANCE BANK WAANZISHA AKAUNTI YA “BARAKA JUNIOR” KWA AJILI YA WATOTO

ACCSESS MICROFINANCE BANK WAANZISHA AKAUNTI YA “BARAKA JUNIOR” KWA AJILI YA WATOTO

Sijaona Saimon Afisa Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Mcrofinance  leo akikabidhi vifaa mbalimbali ikiwemo madaftari, kalamu na Lura kwa Hafsa Athman Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Makumbusho jijini Dar es Salaam, vifaa hivyo vimetolewa kwa shule hiyo ikiwa ni maadhimisho ya benki hiyo kutimiza miaka 15 ya huduma zake nchini kutoka kulia ni Mariam Juma Mratibu wa Nyaraka Benkii ya Access  na Mwalimu Venancia Kahwemama.

Sijaona Saimon Afisa Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Mcrofinance leo akikabidhi vifaa mbalimbali ikiwemo madaftari, kalamu na Lura kwa Hafsa Athman Mwalimu Mkuu Msaidizi wa Shule ya Msingi Makumbusho jijini Dar es Salaam, vifaa hivyo vimetolewa kwa shule hiyo ikiwa ni maadhimisho ya benki hiyo kutimiza miaka 15 ya huduma zake nchini kutoka kushoto ni Nicholaus Makunza Afisa Mikopo Benki ya Access.

Picha ikionesha wafanyakazi wa Benki ya Access wakiwa katika picha ya pamoja na walimu wa shule ya msingi Makumbusho mara baada ya kukabidhi vifaa hivyo.

Nicholaus Makunza Afisa Mikopo Benki ya Access akigawa vifaa hivyo kwa wanafunzi wa shule ya msingi Makumbusho. jijini Dar es Salaam.

Mariam Juma Mratibu wa Nyaraka Access Bank na Hellen Lundalunda Afisa mauzo wakigawa vifaa mbalimbali wa wanafunzi wa shule ya msingi Makumbusho mara baada ya vifaa hivyo kukabidhiwa na benki ya Access.

Picha zikionesha wanafunzi wa shule ya msingi Makumbusho jijini Dar es Salaam wakionesha vifaa mbalimbali kwa ajili ya kusomea mara baada ya kukabidhiwa na benki ya Access ya jijini Dar es Salaam leo.

Access Microfinance Bank imeanzisha akaunti mpya ambayo wameipa jina la “Baraka Junior Account” ambapo wazazi watakuwa wanawawekea watoto wao akiba kidogo kidogo huku wakieleza kwamba akaunti hiyo inakuwa haina makato wala gharama za mwezi za kuiendeshe.

Hayo yamesemwa na Sijaona Saimon Afisa Masoko Mwandamizi wa Benki ya Access Mcrofinance Finance leo alipokuwa anaongea na waandishi wa habari mara baada kutoa msaada wa vifaa mbali mbali katika shule ya msingi Makumbusho ikiwa ni mkakati wa benki hiyo  kutoa shukurani kwa jamii ikielekea kufikisha miaka kumi na tano(15) ya kutoa huduma hapa nchini tangu ilipoanzishwa rasmi.

“Leo tumeamua kuja hapa makumbusho shule ya msingi kutoa vifaa vya shule ambapo tumetoa madaftari pisi elfu moja(1000) Rula elfu moja(1000) na kalamu elfu moja(1000) kwa ajili ya kushiriki baraka na kurudisha kwa jamii ambapo tumelenga upande huu wa Elimu mahsusi kwa sababu tunaamini kupitia hawa wanafunzi baadae tutapata wafanyakazi wa maeneo mbalimbali na viongozi wa nchi yetu pamoja na wafanyabiashara,” amesema Sijaona Simon

Aidha Sijaona Saimon akizungumza kwa niaba ya benkihiyo  amewashukuru Watanzania kwa kuendelea kuwaunga mkono kwa kuendelea kutumia huduma za benki hiyo hapa nchini jambo linalowafanyakuendelea kukua na kuongeza huduma  za kifedha katika maeneo mbalimbali nchini.

Previous articleWANAFUNZI 191 AMBAO HAWAJFANYA MTIHANI KIDATO CHA PILI KUSAKWA NYANG’HWALE.
Next articleMAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 15-2022
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here