Home SPORTS VOLLEYBALL WAIWAKILISHA VYEMA NCHIMICHUANI YA KANDA YA TANO BURUNDI.

VOLLEYBALL WAIWAKILISHA VYEMA NCHIMICHUANI YA KANDA YA TANO BURUNDI.

 

Timu za Tanzania mchezo wa Volleball zimeiwakilisha vyema nchi katika michuano ya kufuzu Kanda ya tano Kwa vijana Chini ya miaka 19 (wavulana) na 18 (wasichana) iliyofanyika kuanzia tarehe 10  na kuhitimishwa jana Bujumbura nchini  Burundi.

Katika michuano hiyo Tanzania imefanikiwa kushika nafasi ya pili (2) na ya tatu (3) kutokana na timu mbili za wanaume zilizoiwakilisha nchi na kupewa majina ya Tanzania One (1) na two (2), huku nafasi ya kwanza ikinyakuliwa na mwenyeji Burundi timu ya pili (2)

Michuano hiyo ilihusisha nchi tatu (3) Tanzania, Rwanda na mwenyeji  Burundi ambapo kila nchi ilipaswa kuwakilishwa na timu 4 (2 kila Jinsia) hukuTanzania ikifanikiwa kupeleka timu 2 zote za jinsia moja ya kiume. 

Akizungumzia mashindano hayo kwa simu Katibu Msaidizi na kocha aliyeenda na wachezaji hao Shukuru Ally amewapongeza wachezaji kujitoa kwa kuiwakilisha nchi kwa ushindi huo na kusema kuwa mashindano mengine watajipanga vyema zaidi na watapeleka wachezaji wa jinsia zote.

Previous articleWAZIRI MKUU MAJALIWA AKIWA BUNGENI LEO DODOMA
Next articleSHAKA ASEMA UONGOZI WA RAIS SAMIA UNASIMAMIA MISINGI YA HAKI, DEMOKRASIA NA UTAWALA BORA
Hughes Dugilo is a Writer, News Producer, Video-Photographer Journalist, and Video Editor experienced for 20 years now performing in News, Documentary, Advertisements and Television Programs. Aside from all above he own and operate his Blog known as Green Waves Media TZ since 2018.

LEAVE A REPLY

Please enter your comment!
Please enter your name here